IQNA

Teknolojia

Kongamano Mauritania lajadili matumizi ya Akili Mnemba katika kuhudumia Qur’ani Tukufu

14:43 - April 13, 2025
Habari ID: 3480535
IQNA – Kongamano lililopewa jina “Jinsi ya kutumia Akili Mnemba (Artificial Intelligence-AI-) kuhudumia Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kuwasaidia Ndugu Zetu wa al-Quds” iliandaliwa nchini Mauritania.

Tukio hilo liliandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Maendeleo ya Njia za Kiuchumi (Development Corridors) cha Mauritania na Shirika la Ujenzi kwa Maendeleo Endelevu la Mauritania.

Ruqayya bint Munayya, mtaalamu katika uwanja wa Akili Mnemba, alizungumza kuhusu matumizi ya teknolojia hiyo katika kuhudumia Qur’ani Tukufu.

Semina hiyo ilifanyika wakati wa hafla maalum katika mji mkuu wa Nouakchott ya kuwaenzi walimu na wahifadhi wa Qur’ani.

Ahmed Jadu Ould Eemi, msemaji wa taasisi mbili zilizoratibu hafla hiyo, alielezea tukio hilo kama kilele cha ratiba za mwezi wa Ramadhani, na kuongeza kuwa kuwaenzi wahifadhi wa Qur’ani kunawatia moyo na kuimarisha harakati za Qur’ani.

Mohamed Al-Amin Ould Sheikhna, mkurugenzi wa Mwongozo wa Kiislamu katika Wizara ya Masuala ya Kiislamu, alisifu kazi ya chama hicho katika kuwaunga mkono wahifadhi wa Qur’ani.

Katika hafla hiyo, walimu na wahifadhi 37 wa Qur’ani wanawake walipewa heshima, na zawadi zilitolewa kwa washindi wa mashindano ya Qur’ani ya Ramadhani.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wawakilishi wa Wizara ya Masuala ya Kijamii ya Mauritania, pamoja na wabunge, mameya, mawakili, na wanaharakati wa jamii.

3492656

Habari zinazohusiana
captcha