IQNA

Kozi ya Kuhifadhi Qur'ani Katika Al Masjid An Nabawi, Madina

17:21 - April 26, 2025
Habari ID: 3480597
IQNA – Kozi ya kina ya mapitio kwa wanaohifadhi Quran Tukufu ilifanyika katika Msikiti wa Mtume, Al Masjid An Nabawi, huko Madina.

Urais wa Masuala ya Kidini katika Misikiti Miwili Mitakatifu (ya Makkah na Madina) umeandaa mpango huu siku ya Ijumaa na Jumamosi, Aprili 25-26. 

Lengo la mpango huu lilikuwa kuwawezesha wanaohifadhi Qur'ani kupitia aya walizozihifadhi katika mazingira ya kujifunza ya kiroho.  Vipindi hivi vya mapitio makubwa ya Qur'ani vilifanyika katika sehemu tatu: Kuhifadhi Qur'ani yote, kuhifadhi Juzuu 20 (sehemu), na kuhifadhi Juzuu 10.

Kozi hizi zimefanyika baada ya sala za asubuhi, adhuhuri, alasiri, magharibi, na isha katika msikiti mtakatifu.

Qur'ani Tukufu ndiyo Andiko la Kidini pekee linalohifadhiwa na wafuasi wake. Watu wasiohesabika katika kila jamii za Kiislamu duniani kote wamehifadhi Qur'an Tukufu kikamilifu tangu siku ya kwanza ilipoteremshwa. 

Qur'ani Tukufu ina Juzuu (sehemu) 30, Surah 114 (sura) na aya 6,236.

3492835

Kishikizo: madina qurani tukufu
captcha