IQNA

Washindi wa Mashindano ya Qur’ani Tukufu Qatar

13:54 - November 27, 2025
Habari ID: 3481574
IQNA – Washindi wa Mashindano ya 30 ya Qur’ani Tukufu ya Sheikh Jassim bin Muhammad bin Thani nchini Qatar wametangazwa katika hafla maalum iliyofanyika Jumanne jijini Doha.

Katika hafla hiyo, Wizara ya Awqaf (Wakfu)  na Mambo ya Kiislamu ya Qatar iliwatunuku washindi wa nafasi tano za juu kwa wanaume katika makundi matatu: raia wa Qatar, mahafidh wa kipekee, na mahafidh wa jumla katika kipengele cha kuhifadhi Qur’ani Tukufu

Hafla ilihudhuriwa na Waziri wa Awqaf na Mambo ya Kiislamu, Ghanem bin Shaheen Al Ghanem, pamoja na wanazuoni, maimamu, na maqari wa Qur’ani, maafisa wa taasisi za elimu na sayansi, na wageni mashuhuri wa kimataifa akiwemo Sheikh Dr. Rushan Abbyasov (Mwenyekiti wa Mashindano ya Qur’ani ya Kimataifa ya Moscow), Mufti Mkuu wa Slovenia Sheikh Nevzet Poric, na Mufti Mkuu wa Croatia Sheikh Aziz Hasanovic.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi, Malallah Abdulrahman Al Jaber, alisisitiza kuwa mashindano haya ni miongoni mwa majukwaa mashuhuri ya Qur’ani katika ulimwengu wa Kiislamu. Alibainisha kuwa idadi ya washiriki mwaka huu ilizidi 2,450, wakiwemo takribani 800 raia wa Qatar.

Washindi wa Kundi la Raia (Qur’ani nzima):

  • Abdulaziz Abdullah Ali Al Hamri – nafasi ya kwanza, zawadi 100,000 Riyal
  • Ibrahim Mohammed Hashem Al Mashhadani – nafasi ya pili, 85,000 Riyal
  • Mohammed Ahmed Mohammed Abdulrahim Al Haram – nafasi ya tatu, 70,000 Riyal
  • Mohammed Abdullah Mohammed Buleidah – nafasi ya nne, 60,000 Riyal
  • Hamad Abdullah Tayis Al Jumaili – nafasi ya tano, 50,000 Riyal

Washindi wa Kundi la Mahafidh wa Kipekee (Qur’ani nzima):

  • Hamza Al Habashi (Marekani) – 100,000 Riyal
  • Mohammed Abdu Ahmed Qasim (Yemen) – 85,000 Riyal
  • Rasheed Abdulrahman Al Alani (Tunisia) – 70,000 Riyal
  • Mahmoud Suleiman Al-Mabruk Idris (Libya) – 60,000 Riyal
  • Magdy Abdullah Salem Ahmed (Misri) – 50,000 Riyal

Washindi wa Kundi la Mahafidh wa Jumla:

  • Nasser Nahed Deeb (Marekani) – 100,000 Riyal
  • Khalid Hafiz Mohammed Fakhrul Huda (Bangladesh) – 85,000 Riyal
  • Saad Abdul-Sattar Abu Saeed (Bangladesh) – 70,000 Riyal
  • Abdulaziz Fahad Mohammed Al Hawsali (Yemen) – 60,000 Riyal
  • Ismail Hafiz Mohammed Elias (Bangladesh) – 50,000 Riyal

Hatua ya mwisho ya mashindano ilifanyika hadharani katika Msikiti wa Imam Muhammad ibn Abdulwahhab, ambapo washiriki 15 kutoka makundi yote walishindana mbele ya Kamati ya Kimataifa ya Waamuzi, iliyoundwa na wanazuoni mashuhuri wa Qur’ani kutoka ulimwengu wa Kiislamu.

Mashindano haya yanabeba heshima kubwa kwa Umma wa Kiislamu, yakisisitiza nafasi ya Qur’ani Tukufu kama mwongozo wa maisha na urithi wa kiroho unaounganisha Waislamu kote duniani, ikiwemo pwani ya Afrika Mashariki ambapo Qur’ani imekuwa nguzo ya elimu, utamaduni na maadili ya jamii.

 3495527

captcha