Muqawama (Mapambano ya Kiislamu)
BEIRUT (IQNA)- Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameongeza kuwa, "Kuhusu kuenea kwa vita, uwezekano huo upo, iwapo watatushambulia, tutalazimika kujihami na tutatumia nguvu zetu zote. Hatuogopi vitisho vya Israel, tunaamini kuwa tutashinda."
Habari ID: 3477901 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Takriban watu 50 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa wakati ndege za kivita za utawala wa Israel zilipodondosha mabomu katika msikiti mmoja katika mtaa wa Sabra katikati mwa Ukanda wa Gaza huku utawala huo ukiendeleza mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina katika eneo hilo.
Habari ID: 3477900 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/16
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA) - Kufuatia mauaji ya hivi sasa yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza, hakutakuwa na nafasi kwa ulimwengu wa Kiislamu kutegemea mazungumzo ya makubaliano na utawala huo, mwanazuoni mmoja wa Kiislamu amesema.
Habari ID: 3477895 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/15
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi wa harakati ya Mapambano ya Kiisalmu (muqawama) ya Ansarullah ya Yemen amezitaka nchi za Kiarabu na Ulimwengu wa Kiislamu kuwa na misimamo ya wazi katika kukabiliana na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
Habari ID: 3477890 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
LONDON (IQNA) - Askofu Mkuu wa Canterbury amesema hakuna msingi wowote wa kimaadili unaoweza kuhalalisha mauaji ya Wapalestina huko Gaza ambayo yanatekelezwa na utawala wa Israel.
Habari ID: 3477889 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Kitendo cha jinai cha Israel cha kulipua makao makuu ya Kamati ya Qatar ya Kujenga upya Gaza kimelaaniwa vikali na mataifa na jumuiya nyingi za Kiarabu na Kiislamu.
Habari ID: 3477888 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) - Mashambulio yasiyokoma ya utawala haramu wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza yaliyoanza tarehe 7 Oktoba yamesababisha hospitali 22 na karibu vituo 50 vya afya katika eneo la pwani kuacha kutoa huduma.
Habari ID: 3477885 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/13
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya utawala wa Kizayuni huko Gaza, kwa wastani, mtoto wa Kipalestina huuawa shahidi kila baada ya dakika 10 katika eneo hilo.
Habari ID: 3477880 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/12
Waungaji mkono Palestina
CAPE TOWN (IQNA) – Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini ulishuhudia maandamano makubwa zaidi katika jiji hilo katika miaka kadhaa wakati makumi ya maelfu ya watu walikusanyika kutan gaza mshikamano na Palestina, wakitaka kukomeshwa kwa ukatili wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3477879 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/12
Diplomasia ya Kiislamu
RIYADH (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika kikao cha pamoja cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kwamba: kadhia ya Gaza ni makabiliano baina ya mhimili wa sharafu au heshima na mhimili wa uovu, na kila mtu anapaswa abainishe yuko upande gani.
Habari ID: 3477878 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/11
Diplomasia ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kikao cha wakuu wa nchi za Kiarabu na Kiislamu kilichofanyika mjini Riyadh, Saudi Arabia kimetilia mkazo ulazima wa kuondolewa mzingiro dhidi ya Gaza na kuingia misafara ya misaada ya kibinadamu katika eneo hilo.
Habari ID: 3477877 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/11
Jinai za Israel
GAZA (IQNA)- Kuendelea mashambulizi ya kila upande ya jeshi la Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza na kujiri mapigano makali kati ya vikosi vya muqawama na wavamizi hao karibu na kambi ya al-Shati iliyoko magharibi mwa mji wa Gaza, ni baadhi ya habari za hivi karibuni kutoka Palestina inayokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel.
Habari ID: 3477873 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/10
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)-Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina amewasilisha faili mbele ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kulalamikia matamshi ya vitisho ya waziri wa utawala wa Kizayuni kwamba ikilazimu, utawala huo haramu utatumia bomu la nyuklia dhidi ya watu wa Gaza.
Habari ID: 3477870 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/10
Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA) - Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, nchi zinazoinukia kiuchumi na nchi zinazoendelea zina uwezo mkubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote katika kuchangia msingi wa mfumo mpya wa dunia.
Habari ID: 3477868 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/10
Jinai za Israel
PRETORIA (IQNA)-Afrika Kusini imeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) yenye makao yake makuu mjini The Hague (ICC) kuuwajibisha utawala wa Kizayuni wa Israel kutokana na vitendo vyake vya ukiukaji wa sheria za kimataifa wakati utawala huo ukiendelea kufanya jinai dhidi ya binadamu katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477867 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/09
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA) - Mwandishi mwingine wa habari wa Kipalestina ameuawa katika mashambulizi ya anga ya Israel huko Gaza huku vita vya utawala haramu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza vikiendelea kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja.
Habari ID: 3477860 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/08
Kimbunga cha Al Aqsa
BEIRUT (IQNA) - Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) ya Hizbullah ya Lebanon amesema Operesheni ya Kimbunge cha al-Aqsa kama kielelezo cha ujasiri, na uchamungu waa watu wa Palestina.
Habari ID: 3477859 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/08
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Utawala wa Kizayuni wa Israel hadi sasa umeshambulia na kuharibu kabisa kwa mabomu misikiti 56 tokea unazish vita vya maangamizi ya umati dhidi ya Ukanda wa Gaza. Aidha misikiti mingine zaidi ya 192 imepata hasara kwa kuharibiwa katika mashambulizi hayo ya kinyama.
Habari ID: 3477855 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/07
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema machaguo yote dhidi ya utawala haramu wa Israel yapo mezani, huku akiuasa utawala huo wa Kizayuni usitishe mara moja uvamizi na mashambulizi yake ya kinyama dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477836 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03
Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA)- Akizungumza leo katika sala ya Ijumaa ya mjini Tehran, Hujjatul Islam wal Muslimeen Kazem Sediqi amesema kuwa leo mrengo wa mapambano ya Kiislamu ni mrengo wa kimataifa na kuongeza kwamba mrengo huo umabadilisha dunia.
Habari ID: 3477832 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03