Diplomasia ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi amewaandikia barua wakuu na viongozi wa nchi 50 duniani kuwahimiza kuwa na kauli moja kuhusu wajibu wa kukomeshwa jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wa Gaza.
Habari ID: 3477919 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/20
Watetezi wa Palestina
CANBERRA (IQNA) – Maelfu ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina waliandamana kote Australia wikiendi hii, wakitoa wito wa kukomeshwa mara moja kwa mashambulizi ya kinyama ya utawala haramu wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza ambayo yameua zaidi ya watu 13,000, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto, tangu Oktoba 7.
Habari ID: 3477918 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/20
Jinai za Israel
RABAT (IQNA) - Shirika la Kiislamu la Elimu, Sayansi, na Utamaduni (ISESCO) limetoa tamko kali siku ya likilaani mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya shule mbili kaskazini mwa Ukanda wa Gaza kuwa ni "fedheha kwa ubinadamu" na "uhalifu wa kutisha".
Habari ID: 3477917 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/20
Watetezi wa Wapalestina
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: kadhia za Gaza zimewadhihirishia walimwengu hakika nyingi zilizofichika, na moja wapo ya hakika hizo ni uungaji mkono wa viongozi wa nchi za Magharibi kwa ubaguzi wa rangi.
Habari ID: 3477916 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/19
Watetezi wa Palestina
TEHRAN (IQNA)- Watu wa Iran ya Kiislamu jana Jumamosi walishiriki katika maandamano makubwa kote nchini kuwatetea watoto wanaoendelea kuuawa wa Palestina sambamba na kulaani "mauaji ya watoto wachanga", "uhalifu", "mauaji ya kimbari", "mauaji ya halaiki", "ugaidi", "uhalifu wa kivita" na "maafa ya binadamu" yanayoendelea katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477915 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/19
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) - Msikiti wa Jamia wa Omari, ambao ni moja ya misikiti mikongwe zaidi katika Jiji la Kale la Gaza, uliripotiwa kulengwa katika mashambulizi ya anga ya utawala katili wa Israel siku ya Alhamisi.
Habari ID: 3477910 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/18
Jinai za Israel
GAZA (IQNA)- Utawala haramu wa Israel umeua shahidi zaidi ya Wapalestina 12,000, wakiwemo watoto wasiopungua 5,000 tokea uanzishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 7.
Habari ID: 3477908 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/18
Diplomasia
TEHRAN (IQNA)- Uzembe wa Umoja wa Mataifa na hasa mkwamo katika Baraza la Usalama la umoja huo ambao una jukumu muhimu la kulinda amani na usalama wa kimataifa, kuhusu vita vya Gaza, jinai za kivita na mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni, umekosolewa vikali kimataifa.
Habari ID: 3477904 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17
Jinai za Israel Gaza
TEHRAN (IQNA)- Wataalam wa Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa Jumuiya ya kimataifa kuzuia mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Palestina wa Gaza huku utawala katili wa Israel ukiendeleza vita vyake dhidi ya eneo hilo lililozingirwa.
Habari ID: 3477903 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17
Muqawama (Mapambano ya Kiislamu)
BEIRUT (IQNA)- Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameongeza kuwa, "Kuhusu kuenea kwa vita, uwezekano huo upo, iwapo watatushambulia, tutalazimika kujihami na tutatumia nguvu zetu zote. Hatuogopi vitisho vya Israel, tunaamini kuwa tutashinda."
Habari ID: 3477901 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Takriban watu 50 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa wakati ndege za kivita za utawala wa Israel zilipodondosha mabomu katika msikiti mmoja katika mtaa wa Sabra katikati mwa Ukanda wa Gaza huku utawala huo ukiendeleza mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina katika eneo hilo.
Habari ID: 3477900 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/16
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA) - Kufuatia mauaji ya hivi sasa yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza, hakutakuwa na nafasi kwa ulimwengu wa Kiislamu kutegemea mazungumzo ya makubaliano na utawala huo, mwanazuoni mmoja wa Kiislamu amesema.
Habari ID: 3477895 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/15
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi wa harakati ya Mapambano ya Kiisalmu (muqawama) ya Ansarullah ya Yemen amezitaka nchi za Kiarabu na Ulimwengu wa Kiislamu kuwa na misimamo ya wazi katika kukabiliana na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
Habari ID: 3477890 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
LONDON (IQNA) - Askofu Mkuu wa Canterbury amesema hakuna msingi wowote wa kimaadili unaoweza kuhalalisha mauaji ya Wapalestina huko Gaza ambayo yanatekelezwa na utawala wa Israel.
Habari ID: 3477889 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Kitendo cha jinai cha Israel cha kulipua makao makuu ya Kamati ya Qatar ya Kujenga upya Gaza kimelaaniwa vikali na mataifa na jumuiya nyingi za Kiarabu na Kiislamu.
Habari ID: 3477888 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) - Mashambulio yasiyokoma ya utawala haramu wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza yaliyoanza tarehe 7 Oktoba yamesababisha hospitali 22 na karibu vituo 50 vya afya katika eneo la pwani kuacha kutoa huduma.
Habari ID: 3477885 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/13
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya utawala wa Kizayuni huko Gaza, kwa wastani, mtoto wa Kipalestina huuawa shahidi kila baada ya dakika 10 katika eneo hilo.
Habari ID: 3477880 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/12
Waungaji mkono Palestina
CAPE TOWN (IQNA) – Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini ulishuhudia maandamano makubwa zaidi katika jiji hilo katika miaka kadhaa wakati makumi ya maelfu ya watu walikusanyika kutan gaza mshikamano na Palestina, wakitaka kukomeshwa kwa ukatili wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3477879 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/12
Diplomasia ya Kiislamu
RIYADH (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika kikao cha pamoja cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kwamba: kadhia ya Gaza ni makabiliano baina ya mhimili wa sharafu au heshima na mhimili wa uovu, na kila mtu anapaswa abainishe yuko upande gani.
Habari ID: 3477878 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/11
Diplomasia ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kikao cha wakuu wa nchi za Kiarabu na Kiislamu kilichofanyika mjini Riyadh, Saudi Arabia kimetilia mkazo ulazima wa kuondolewa mzingiro dhidi ya Gaza na kuingia misafara ya misaada ya kibinadamu katika eneo hilo.
Habari ID: 3477877 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/11