Kadhia ya Palestina.
IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amesema mpaka wa ulimwengu wa Kiislamu uko Gaza hivi leo, na kwamba Wapalestina wa eneo hilo wamesimama dhidi ya kiburi au mfumo wa kiistikbari na Marekani.
Habari ID: 3478140 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/03
Jinai za Israel
IQNA - Zaidi ya maeneo 200 ya kiakiolojia na ya kale katika Ukanda wa Gaza yameharibiwa na uvamizi wa kijeshi wa Israel tangu Oktoba 7, kulingana na mamlaka huko Gaza.
Habari ID: 3478117 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/31
Waislamu Marekani
IQNA - Baadhi ya viongozi wa Kiislamu wa Marekani wanaripotiwa kusita kufanya kazi na Ikulu ya White House katika kuandaa mkakati wa kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) kutokana na utawala wa Rais Joe Biden kuendelea kuunga mkono vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na Israel dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
Habari ID: 3478109 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/29
Watetezi wa Palestina
IQNA - Waandamanaji kutoka matabaka mbalimbali walifanya maandamano mjini The Hague, Uholanzi kudai haki kwa Wapalestina na uchunguzi wa jinai zinazofanywa na utawala wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3478106 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/28
IQNA-Rais Miguel Diaz-Canel wa Cuba amelaani vikali mauaji ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza na kueleza kwamba, mauaji hayo ya kimbari ni kashfa na fedheha kwa ubinadamu.
Habari ID: 3478104 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/28
Watetezi wa Palestina
IQNA - Mikutano ya hadhara imefanyika katika miji katika nchi mbalimbali za Magharibi mwishoni mwa juma kupinga mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Gaza na kutaka kuwasilishwa kwa misaada ya kibinadamu katika eneo lililozingirwa.
Habari ID: 3478086 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/24
Kadhia ya Palestina
IQNA-Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hatimaye limepitisha azimio kuhusu jinai za Israel dhidi ya Gaza, likidai kuongezwa kwa misaada katika eneo lililozingirwa lakini lakini limeshindwa kuulazimisha utawala haramu wa Israel usitishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika eneo hilo.
Habari ID: 3478078 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/23
Watetezi wa Palestina
IQNA - Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Ansarullah nchini Yemen imetan gaza kuanza mchakato wa uhamasishaji wa vijana wanaojitolea kuenda kupigana katika vita vya Gaza pamoja na wapiganaji wa harakati za Kiislamu huko Palestina.
Habari ID: 3478070 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/21
Mapambano ya Wapalestina
IQNA - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) ya Palestina, Hamas, Ismail Haniya amesisitiza uthabiti na azma la harakati hiyo katika kuendeleza mapambano ya kupigania ukombozi wa Palestina.
Habari ID: 3478066 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/20
IQNA Ripoti ya kutisha iliyotolewa na Wizara ya Afya ya Palestina, imefichuliwa kuwa wakati wa hujuma za hivi karibuni za kijeshi za utawala wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza, asilimia 70 ya watu 18,800 waliouawa walikuwa wanawake na watoto.
Habari ID: 3478053 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/18
Watetezi wa Palestina
IQNA - Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Kibinadamu ya Kiislamu yenye makao yake London (IHRC) amekosoa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa undumilakuwili wake linapokuja suala la kushtaki wahusika wa uhalifu wa kivita.
Habari ID: 3478050 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/17
Watetezi wa Palestina
IQNA – Toleo la 19 la Jukwaa la Kimataifa la Russia na Ulimwengu wa Kiislamu lilifanyika mjini Moscow huku wazungumzaji wakizingatia hali mbaya ya Gaza.
Habari ID: 3478028 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/13
Matukio ya Palestina
IQNA- Idara ya Habari ya Serikali ya Gaza imeripoti kwamba asilimia 61 ya nyyumba za raia wa Kipalestina huko Ukanda wa Gaza zimebomolewa katika vita vya maangamizi ya umati vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo lilolozingirwa.
Habari ID: 3478026 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/12
Jinai za Israel
IQNA- Mwanaharakati wa haki za binadamu mwenye makao yake mjini London, Uingereza anasema jibu la nchi za Magharibi kwa mauaji ya kimbari yanayoendelea kutekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Gaza kwa mara nyingine tena limefichua "uongo" wao kuhusu kujali haki za binadamu.
Habari ID: 3478015 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/10
Jinai za Israel
NEW YORK (IQNA)- Marekani, ambayo ni mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, imetumia kura yake ya turufu kupinga azimio lililopendekezwa na UAE la kuanzisha usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478009 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/09
Watetezi wa Palestina
TEHRAN (IQNA)-Imamu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran ameashiria mpango wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kutatua kadhia ya Palestina kwa njia ya kura ya maoni kwa msingi wa "kila Mpalestina ana kura moja", na kusema: Maneno yetu ni ya kimantiki na ya kidemokrasia.
Habari ID: 3478008 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/08
Jinai za Israel
GAZA (IQNA)-Harakati ya Kiisalmu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas, imelaani vikali vikosi vya utawala haramu kwa kuwakamata na kuwanyang'anya mali raia waliokimbia makazi yao katika shule moja katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478007 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/08
Jinai za Israel
GAZA (IQNA) - Msikiti wa kihistoria wa Othman bin Qashqar, ulioko katika Jiji la Kale la Gaza ulilipuliwa kwa mabomu yaliyodondoshwa na ndege za kivita za utawala haramu Israel siku ya Alhamisi, na kusababisha Wapalestina kadhaa kuuawa shahidi na uharibifu wa nyumba zilizo karibu, shirika rasmi la habari la Palestina WAFA liliripoti.
Habari ID: 3478005 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/08
Diplomasia
MOSCOW (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa wito wa kusitishwa mara moja jinai za Israel za "mauaji ya kimbari" dhidi ya Wapalestina Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478004 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/08
Watetezi wa Palestina
DOHA – IQNA: Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (IUMS) umetoa wito wa kufanyika maandamano na mikutano kote duniani Ijumaa hii kuunga mkono Wapalestina wanakandamizwa Gaza na Msikiti wa Al-Aqsa mjini Quds (Jerusalem) sambamba na kulaani utawala wa dhalimu wa Israel.
Habari ID: 3478000 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/07