IQNA

Raia wa Malaysia waazimia kutetea Wapalestina wanaokandamizwa

20:47 - November 20, 2023
Habari ID: 3477920
KUALA LUMPUR (IQNA) – Mkutano ulifanyika katika Msikiti wa Sultan Iskandar ulioko Bandar Dato' Onn huko Johor, Malaysia, Jumapili jioni kwa ajili ya mshikamano na watu wa Palestina.

Zaidi ya Waislamu 5,000, wakiwa wamevalia mavazi meupe, waliwasili mapema saa tisa alasiri, wengine wakiwa wanpeperusha bendera za Palestina kama ishara ya mshikamano na Wapalestina waliozingirwa katika Ukanda wa Gaza.

Khatibu wa Johor Onn Hafiz Ghazi amesema uungaji mkono wa umati huo mkubwa unaonyesha azma yao ya kuwatetea Wapalestina ambao wanakabiliwa na hujuma ya kinyama ya utawala haramu wa Israel na kuongoza kuwa ni  haki yao ya kusikilizwa na kila mtu hasa katika jukwaa la kimataifa.

"Sababu ya kukusanyika hapa kama 'Bangsa Johor' ni kutoa msaada wetu usiogawanyika kwa Waislamu wenzetu huko Palestina.

"Pia tunawataka viongozi wa dunia kurejesha haki za kibinadamu kwa Wapalestina na mamlaka ya Palestina kurejeshwa. Pia tunataka kusitishwa kwa mauaji ya kikatili na ya kinyama yanayotokea huko.

"Nilijulishwa siku mbili zilizopita kwamba kuna mwanafunzi hakuhudhuria darasa  kwani watu 44 wa familia yake waliuawa huko Palestina na hii ndiyo hali ya Palestina," alisema wakati wa hotuba yake. mbele ya katibu wa jimbo la Johor Tan Sri Datuk Dk Azmi Rohani, mwenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Kiislamu ya Johor Mohamad Fared Mohd Khalid,  Datuk Hasni Mohamad na Dk Sahruddin Jamal na wageni wengine.

Pia aliwasilisha hundi ya zaidi ya RM2.5 milioni katika michango iliyokusanywa kutoka misikiti na suraus (maeneo ya kidini), pamoja na makampuni yanayohusiana na serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali huko Johor, ambayo yataelekezwa kwa Mfuko wa Kibinadamu wa Palestina wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Malaysia. 

/3486090

Habari zinazohusiana
captcha