Watetezi wa Palestina
DOHA – IQNA: Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (IUMS) umetoa wito wa kufanyika maandamano na mikutano kote duniani Ijumaa hii kuunga mkono Wapalestina wanakandamizwa Gaza na Msikiti wa Al-Aqsa mjini Quds (Jerusalem) sambamba na kulaani utawala wa dhalimu wa Israel.
Habari ID: 3478000 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/07
Watetezi wa Palestina
KARBALA (IQNA) - Sheikh Abdul Mahdi al-Karbalayi, mwakilishi wa Ayatullah Sayyed Ali al-Sistani jijini Karbala, Iraq amesisitiza uungaji mkono kwa watu wa Palestina katika kukabiliana na uchokozi wa kikatili wa utawala wa Kizayuni.
Habari ID: 3477995 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/06
Jinai za Israel
BEIT LAHM (IQNA)- Kanisa moja la Palestina limeamua kuweka kunyesha magofu ya nyumba zilizobomolewa badala ya Mti wa Krismasi kama ilivyo ad ana kusema kuwa hakuna cha kusherehekea wakati huu utawala haramu wa Israel unapendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3477989 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/05
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Huku vita vya maangamizi ya kimbari vya utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Gaza vikiendelea, maafisa wa Palestina wanasema ndege za kivita za utawala huo zimelenga maeneo ya karibu na mji wa Khan Yunis kwa kutumia mabomu ya fosforasi ambayo yanakatzwa kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
Habari ID: 3477988 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/05
Jinai za Israel
CAIRO (IQNA)- Sheikh Mkuu wa Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar cha Misri amesema kuwa wakati umefika sasa wa kusitishwa jinai za utawala gaidi wa Israel na mauaji ya watu katika ardhi ya Palestina.
Habari ID: 3477985 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/04
Jinai za Israel
WASHINGTON, DC (IQNA) - Viongozi wa Kiislamu kutoka majimbo kadhaa ya yanayoamua matokeo ya uchaguzi Marekani, yaani Swing States, wametan gaza kuondoa uungaji mkono wao kwa Rais Joe Biden, kwa sababu ya kushindwa kwake kutoa wito wa kusitishwa kwa mapigano huko Gaza.
Habari ID: 3477981 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/03
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) - Idadi ya misikiti iliyoharibiwa kabisa na utawala wa Israel katika vita vyake dhidi ya Gaza iliongezeka hadi 88 siku ya Ijumaa, huku usitishaji vita mfupi ukimalizika na utawala wa Kizayuni kuanza tena uchokozi wake mbaya.
Habari ID: 3477975 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/02
Jinai za Israel
OTTAWA (IQNA) - Zaidi ya waandamanaji 100 Waislamu walikusanyika karibu na ubalozi wa Israel katika mji mkuu wa Marekani siku ya Ijumaa na kusali sala ya Ijumaa hapo sambamba na kulaani mashambulizi yanayoendelea ya utawala haramu wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477973 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/02
Jinai za Israel
UKINGO WA MAGHARIBI (IQNA)- Watoto wawili wa Kipalestina wameuawa shahidi kwa kupigwa risasi na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika mji wa Jenin, kaskazini ya eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Habari ID: 3477969 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/30
Watetezi wa Palestina
CAIRO (IQNA) - Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar cha Misri kimesema wakati umefika kwa watu wote wanaopenda uhuru duniani kuungana kwa ajili ya kuundwa taifa huru la Palestina ili kukomesha ubeberu na ukaliaji mrefu zaidi wa ardhi ya wengine katika historia.
Habari ID: 3477968 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/30
Waungaji mkono Palestina
TEHRAN (IQNA)- Katika muendelezo wa himaya na uungaji mkono wa ulimwengu kwa mapambano ya wananchi wa Gaza na kulaani jinai za utawala ghasibu wa Israel, maelfu ya wananchi wa Pakistan wameandamana na kuelekea katika ubalozi mdogo wa Marekani.
Habari ID: 3477967 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/30
Kimbunga cha Al Aqsa
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei anasema tukio la kihistoria la Kimbunga cha al-Aqsa cha harakati ya Hamas kimsingi lilikuwa dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel, lakini limeweza kuvuruga sera za Marekani katika eneo la Magharibi mwa Asia na litaifuta kabisa ajenda hiyo.
Habari ID: 3477965 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/29
Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA)- Kutokana na udharura na haja ya kuongezwa na kuimarishwa umoja na mshikamano baina ya wapenda uhuru na wapigania haki hususan nchi za Kiislamu katika kuilaani Israel, Waziri Mkuu wa zamani wa Malaysia, Mahathir Mohammad amesema: “Kwa mujibu wa Qur’ani Tukufu, ili nchi za Kiislamu zimshinde Mzayuni na adui wao wa pamoja hazina njia nyingine ghairi ya kudumisha umoja, kuimarisha msingi wa ulinzi na nguvu za kijeshi.
Habari ID: 3477964 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/29
Jinai za Israel
Jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limekiri kuwa zaidi ya askari wake 1,000 wa walowezi wa utawala huo waliuawa wakati wa mapigano ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
Habari ID: 3477959 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/28
Waislamu Ujerumani
BERLIN (IQNA) – Kiongozi mmoja wa jamii ya Waislamu nchini Ujerumani ameelezea wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa chuki dhidi ya Waislamu nchini humo kufuatia vita vya utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
Habari ID: 3477958 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/28
Jinai Marekani
VERMONT (IQNA) - Polisi wa Jimbo la Vermont waliripoti Jumapili kwamba vijana watatu wa Kipalestina walipigwa risasi na kujeruhiwa karibu na Chuo Kikuu cha Vermont.
Habari ID: 3477954 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/27
Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa
TEHRAN (IQNA)- Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, Harakati ya Kiislamu (Muqawama) ya Kupigania Ukombozi wa Palestina (HAMAS) ilivunja mgongo wa Israel kwa kutegemea imani na ushujaa katika operesheni ya kimbunga ya Al-Aqswa.
Habari ID: 3477938 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/24
Watetezi wa Palestina
TUNIS (IQNA) - Rached Ghannouchi, mkuu wa Chama cha Ennahda cha Tunisia, alielezea Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa kama zawadi kwa Umma wa Kiislamu.
Habari ID: 3477934 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/23
Mapambano dhidi ya Israel
SANAA (IQNA) - Yemen imevurumisha makombora ya cruise dhidi ya maeneo ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel
Habari ID: 3477933 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/23
Harakati za Mapambano ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Hizbullah jana Jumatano alikutana na ujumbe wa maafisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS mjini Beirut kujadili matukio ya Gaza, huku idadi ya wananchi wa Palestina waliouawa shahidi kwenye mashambulizi ya kikatili ya Israel katika eneo hilo linalokaliwa kwa mabavu ikikaribia 15,000.
Habari ID: 3477931 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/23