IQNA

Mfalme wa Malaysia aamuru shughuli zisitishwe misikitini

20:39 - March 17, 2020
Habari ID: 3472574
TEHRAN (IQNA) – Harakati zote misikitini nchini Malayasia, ikiwa ni pamoja na sala za Ijumaa, zimesitishwa kwa muda wa siku kumi kufuatiia amri ya mfalme wa nchi hiyo ili kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama kirusi cha corona.

Kwa mujibu wa waziri anayeshughulikia  masuala  ya kidini Dr. Zulkifli Mohammad al-Bakri, “shughuli zote za misikiti, ikiwa ni pamoja na sala ya Ijumaa na sala za jamaa zimesimamishwa kwa muda kuanzia Machi 17 hadi 26.” Amesema wamechukua uamuzi huo kufuatia ushauri wa wizara ya afya. Amesema kwa mujibu wa ushauri wa mwaka 2015 wa Kamati ya Fatwa, iwapo Muislamu nchini humo atafariki kutokana na COVID-19 mwili tayammum itafanywa juu ya mfuko uliko mwili.

Hadi sasa kuna watu 553 waliomabukizwa corona nchini Malaysia na miognoni mwao mtu moja, aliyekuwa na umri wa miaka 60, amefariki.

3470935

captcha