Erekat ambaye alipata umashuhuri kama mwakilishi wa Palestina katika mazungumzo ya kimataifa ameaga dunia hospitalini akiwa na umri wa miaka 65. Kifo chake kimetangazwa kupitia taarifa ya Chama chake cha Fatah.
Erekat alishiriki katika takriban juhudi zote za kusaka amani kati ya utawala haramu wa Israel na Wapalestina, kuanzia mkutano wa kihistoria uliofanyika Madrid mwaka 1991, ambapo alihudhuria akiwa amejifunika kitambaa cha kufunga kichwani chenye miraba ya rangi nyeusi na nyeupe ambayo ni ishara ya utaifa wa Wapalestina.