Sherehe ya kufunga Mashindano ya 43 ya Kitaifa ya Qur'ani ya Iran imefanyika katika Hoteli ya Eram mjini Tehran Ijumaa jioni.
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu Iran Sayyed Abbas Salehi na Mkuu wa Shirika la Wakfu na Misaada Iran Hujjatul Islam Sayyed Mehdi Khamoushi. Washiriki katika kategoria mbali mbali walitunukiwa zawadi.