IQNA

Kituo cha Kiislamu Ufaransa kimeandaa mashindano ya mafundisho ya Qur’ani

21:59 - April 16, 2021
Habari ID: 3473821
TEHRAN (IQNA)-Kituo cha Kiislamu nchini Ufaransa kimeandaa mashindano kuhusu mafundisho ya Qur’ani Tukufu.

Kwa mujibu wa taarifa kutakuwa na mashindano manne katika wiki nne za mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Washiriki wanajibu maswali 20 kuhusu maundisho ya Qur’ani Tukufu na pia mafundisho maalumu ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Aidha kwa kuzingatia kuwa mashindano hayo yanafanyika kwa njia ya intaneti, watu kutoka maeneo yote ya dunia na washindi watatangazwa mwishoni mwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

3964204

Kishikizo: ramadhani ufaransa
captcha