IQNA

Qari Al-Karbalaei wa Iraq akisoma Qur'ani mbele ya Maustadh wa Kimisri

20:55 - May 21, 2023
Habari ID: 3477026
TEHRAN (IQNA) – Osama al-Karbalaei ni msomaji mashuhuri wa Qur'ani Tukufu Iraqi na qari wa Haram Takatifu ya Imam Hussein (AS) huko Karbala.


Hivi karibuni alisoma Aya za 81 na 82 za Surah Al-Isra mbele ya maqari kadhaa wa juu wa Misri, akiwemo Ustadh Abdul Fattah Taruti.
Ifuatayo ni klipu ya qiraa yake.

Na sema: Kweli imefika, na uwongo umetoweka. Hakika uwongo lazima utoweke! Na tunateremsha katika Qur'ani yaliyo ni matibabu na rehema kwa Waumini. Wala hayawazidishii madhaalimu ila khasara.

captcha