Ofisi ya Urais Mkuu wa Masuala ya Kidini ya Misikiti Miwili Mitukufu itaendesha madarasa ya Qur'ani, tovuti ya habari ya Sabaq iliripoti kuwa;
Kozi hizo zitakuwa na mafunzo ya usomaji na kuhifadhi Qur’ani kwa wanaume na wanawake.
Kwa mujibu wa maafisa wa urais mkuu, kozi hizo zitaanza tarehe 25 Dhul Hijja mwezi wa Julai tarehe 2 na kuendelea hadi tarehe 19 Muharram mwezi Julai tarehe 25 mwaka huu 2024.
Zitafanyika katika vipindi viwili: baada ya sala ya asubuhi na baada ya sala ya Alasiri.
Swala za Jamaa katika Msikiti wa Mtume Muhammad (SAW)
Usajili wa kozi hizo utaanza siku ya Jumatatu, mwezi Juni, mwaka 2024, kupitia tovuti ya urais mkuu.
Kuandaa mipango na shughuli za Qur’ani kama vile duru na kozi za Qur'ani katika Msikiti wa Mtume Muhammad (saw) na Msikiti Mkuu wa Makka kumeongezeka sana katika miaka ya hivi karibuni.