IQNA

Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Misri yanalenga kuwaenzi wahifadhi

17:36 - December 01, 2024
Habari ID: 3479830
IQNA - Wizara ya Wakfu ya Misri imesema mashindano ya kila mwaka ya kimataifa ya Qur'ani nchini humo yanalenga kuwaenzi wahifadhi Qur'ani na kuimarisha jukumu lao katika kukuza thamani za Qur'ani duniani.

Aidha wizara hiyo  imesema mashindano hayo pia ni mahali pa kukusanyika wanaharakati wakuu wa Qur'ani kutoka duniani kote ili kuonyesha vipaji vyao vya Qur'ani.

Mkutano na waandishi wa habari umefanyika katika msikiti katika Mji Mkuu wa Utawala wa Misri karibu na Cairo siku ya Jumapili ambapo Waziri wa Awqaf Osama el Azhari ametoa maelezo ya toleo la 31 la mashindano hayo.

Wizara ya Waku ilisema hapo awali kwamba jumla ya zawadi za pesa taslimu zitakazogawiwa kati ya washindi wa toleo hili zitafikia pauni milioni 10 za Misri.

3490889

Toleo la 30 la mashindano ya kimataifa ya Qur'ani lilifanyika Aprili 2024 na wahifadhi kutoka nchi 64 walihudhuria.

Walishindana katika kategoria sita, ikiwa ni pamoja na kuhifadhi Qur'ani nzima pamoja na qiraa, na Tafseer (tafsiri), kuhifadhi Qur'ani kwa wasiozungumza Kiarabu, na kuhifadhi Qur'ani kwa viongozi wa maimamu na wahubiri.

Habari zinazohusiana
captcha