IQNA

Video: Mahmoud Shahat Anwar asoma Qur’ani kwenye ufunguzi wa Mashindano ya 32 ya Kimataifa ya Qur’ani Misri

18:29 - December 08, 2025
Habari ID: 3481632
IQNA – Mashindano ya 32 ya Kimataifa ya Qur’ani nchini Misri yamefunguliwa tarehe 6 Disemba 2025 kwa qira’a ya qari mashuhuri wa Misri, Mahmoud Shahat Anwar.

Mashindano ya mwaka huu yamepewa jina la baba yake, marehemu Sheikh Shahat Muhammad Anwar, na yataendelea kuanzia Disemba 6 hadi Disemba 10, 2025.

Katika hafla ya ufunguzi, Anwar alisoma aya ya 23 na 24 za Surah Al-Isra. Waandaaji walisema usomaji wake uliamsha kumbukumbu ya urithi wa qari huyo mashuhuri na kuweka hali ya kiroho kwa tukio hilo.

Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima.

Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.

3495661

captcha