IQNA-Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran imesisitiza kuwa, kuainishwa hatima na kufanya maamuzi kuhusu mustakbali wa Syria ni jukumu la pekee la wananchi wa nchi hiyo bila ya uingiliaji uharibifu wala kulazimishwa na mataifa ya kigeni.

Kwa mujibu wa Idara Kuu ya Habari na masuala ya Usemaji ya Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kuhusiana na matukio ya hivi karibuni ya Syria ambapo huku ikikumbusha msimamo wa kimsingi wa Iran wa kuheshimu umoja, mamlaka ya kitaifa na utimilifu wa ardhi Syria, imeeleza kuwa, kufikiwa jambo hili kunahitaji kuhitimishwa haraka mapigano ya kijeshi, kuzuia vitendo vya kigaidi na kuanza kwa mazungumzo ya kitaifa kwa kushirikishwa matabaka yote ya jamii ya Syria ili kuunda serikali jumuishi ambayo itakuwa na wakilishi wa watu wote wa Syria.
Sehemu nyingine ya taarifa hiyo imeeleza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaunga mkono taratibu za kimataifa zinazoegemezwa kwenye Azimio nambari 2254 la Umoja wa Mataifa la kufuata mchakato wa kisiasa nchini Syria kama ilivyokuwa hapo awali na inaendelea kushirikiana kiujenzi na Umoja wa Mataifa katika suala hili.
4252998