Uvamizi huo, ambao Wapalestina wanauona kama uchokozi wa makusudi, ulikuwa sehemu ya Maandamano ya Mwaka ya Bendera yanayoadhimisha uvamizi wa Israeli wa mwaka 1967 wa mji huo.
Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Palestina, WAFA, kundi hilo la walowezi lilijumuisha waziri wa Kizayuni mwenye misimamo mikali, Itamar Ben-Gvir, pamoja na mkewe na maafisa wengine wa Kizayuni. Tukio hilo liliendeshwa chini ya uangalizi wa jeshi la Israeli, ambalo kwa mujibu wa ripoti, liliwaruhusu kuingia katika eneo hilo kupitia Lango la Wamoroko.
WAFA, ikinukuu vyanzo vya ndani, ilisema kuwa takriban walowezi 1,500 waliingia katika viwanja vya Al-Aqsa na kufanya ibada za Kitalmudi, ambazo zinaonekana kuwa haramu na za kichokozi.
Msikiti wa Al-Aqsa, ulioko Mashariki mwa al-Quds, unaheshimiwa kama sehemu ya tatu takatifu zaidi katika Uislamu baada ya Maka na Madina. Tangu uvamizi wa Israel wa mji huo katika vita vya mwaka 1967, eneo hilo limeendelea kuwa kitovu cha mvutano wa kidini na kisiasa. Ingawa ziara za wasiokuwa Waislamu zinaruhusiwa chini ya makubaliano ya hali ya sasa (status quo), sala za wasiokuwa Waislamu zimepigwa marufuku rasmi , sheria ambayo wachunguzi wanasema inavunjwa kwa kuungwa mkono kwa kificho na mamlaka za Israel.
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imelaani uvamizi huo wa walowezi na kuutaja kuwa ni “ukiukwaji wa wazi wa utakatifu na hadhi ya Msikiti wa Al-Aqsa.” Hamas imeahidi kwamba Wapalestina wataendelea kulilinda eneo hilo takatifu na kupinga kwa nguvu yoyote juhudi za kuligawanya au kuligeuza kuwa ya Kiyahudi.
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imeonya kuwa uvamizi huo ulikuwa ni “uenezaji taharuki kwa makusudi” na matusi ya moja kwa moja kwa hisia za kidini za Waislamu duniani kote. OIC imesisitiza kuwa Msikiti wa Al-Aqsa “kwa ukamilifu wake” ni wa ibada ya Waislamu pekee na kuitaka jumuiya ya kimataifa kusitisha ukiukaji unaojirudia wa utakatifu wa eneo hilo.
3493240