IQNA

Jinai za Wazayuni

Walowezi wa Kizayuni wauhujumu Msikiti wa Al Aqsa mara 22 mwezi Desemba

14:21 - January 02, 2025
Habari ID: 3479991
IQNA – Katika mwezi uliopita wa Desemba, kulikuwa na hujuma 22 za walowezi wa Kizayuni dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa  katika mji wa al-Quds (Jerusalem) Mashariki unaokaliwa kwa mabavu.

Hujuma hizo kwa kawaida hufanyika kwa himaya ya jeshi la utawala haramu wa Israel.

Wizara ya Wakfu ya Palestina imetoa taarifa Jumatano ikisema: "Mwezi Desemba kulikuwa na ongezeko la hujuma ya vikosi vya utawala ghasibu wa Israel na walowezi wa Kizayuni dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa."

Taarifa hiyo imesema: "Uvamizi huu unalenga kuunda hali mpya katika msikiti kwa kuruhusu wavamizi kufanya ibada za kidini za Kiyahudi."

Askari wa utawala wa Israel, wizara ilisema, wanatoa ulinzi kwa  wavamizi, wanazuia kazi za walinzi wa msikiti na kuwazuia waumini wa Kiislamu kuingia msikitini hapo.

Jumapili, waziri wa mawasiliano wa Israel Shlomo Karhi, akiwa ameandamana na walowezi wa Kizayuni  walivamia na kuingia kwa lazima katika uwanja wa msikiti huo na kufanya ibada ya Kiyahudi katika eneo la chini ya Ukuta wa Magharibi (Ukuta wa Al-Buraq).

Wiki iliyopita, waziri wa usalama wa kitaifa wa mrengo wa kulia wa Israel Itamar Ben-Gvir alivamia msikiti huo kuadhimisha sikukuu ya Kiyahudi chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Msikiti wa Al-Aqsa ni eneo la tatu takatifu zaidi kwa Waislamu duniani. Wayahudi wanaita eneo hilo kuwa eti ni 'Mlima wa Hekalu', wakisema lilikuwa eneo la mahekalu mawili ya Kiyahudi katika nyakati za kale.

Utawala haramu wa Isarel ulikalia kwa mabavu  al-Quds Mashariki, ambako Al-Aqsa iko, wakati wa Vita vya Waarabu na Israeli vya 1967. Baadaye Israel iliteka  jiji lote mwaka 1980 katika hatua ambayo haijawahi kutambuliwa na jumuiya ya kimataifa.

3491300

Habari zinazohusiana
captcha