
Kwa mujibu wa taarifa iliyonukuliwa na El‑Balad News, mitihani hiyo itafanyika kuanzia Juni 8 hadi Juni 18, 2026.
Wizara imetoa waraka wa dharura kwa idara zake zote ikiagiza kuwajulisha watu wote waliotajwa katika orodha iliyotangazwa wajitokeze katika Msikiti wa Al‑Nour uliopo eneo la Abbasiyya ili kushiriki mitihani ya maandishi ya kitaifa ya mashindano ya mwaka huu.
Wizara imeweka vigezo na masharti madhubuti kwa washiriki. Miongoni mwa masharti hayo ni kwamba mshiriki asiwe na umri zaidi ya miaka 25. Pia waombaji hawapaswi kuwa tayari wamepata nafasi za juu katika matoleo yaliyopita ya mashindano haya ya kimataifa.
Kwa upande wa kitengo cha sita, kinachojulikana kama “Familia ya Qur’ani”, washiriki wanatakiwa wawe wamehifadhi Qur’ani Tukufu nzima kwa riwaya ya Hafs kutoka kwa ‘Asim, Warsh kutoka kwa Nafi‘, au zote mbili. Aidha, wanapaswa kuwa na ufahamu mzuri wa maana za aya pamoja na uelewa wa kina wa makusudio na maudhui ya Qur’ani.
Katika kitengo hiki, idadi ya wanafamilia waliokuwa wahifadhi wa Qur’ani inapaswa kuwa angalau watatu, na familia hiyo isiwe imewahi kushika nafasi za juu katika mashindano hayo hapo awali.
Wizara pia imesisitiza kuwa vipengele vyote vya mashindano viko wazi kwa wanaume na wanawake, mradi mshiriki hajawahi kushinda tuzo ya kwanza katika sehemu yoyote ya mashindano hayo hapo kabla.
Aidha, wizara imeonya kuwa mshiriki yeyote atakayebainika kutokidhi masharti katika hatua yoyote ya mashindano ataondolewa mara moja kwenye ushindani.
3497451