IQNA

Al-Azhar yazindua mpango wa mafunzo ya Qur'ani katika majira ya joto

19:40 - June 01, 2025
Habari ID: 3480774
IQNA – Toleo la tatu la mpango wa majira ya joto wa Qur'ani wa Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar nchini Misri limeanza kutekelezwa Jumapili.

Huu ni mpango maalum wa Qur'ani kwa vituo vinavyohusiana na Al-Azhar na vituo vyote binafsi vya kuhifadhi Qur'ani nchini Misri ambavyo vinafanya kazi chini ya usimamizi wa Al-Azhar.

Mpango huu wa Qur'ani kwa majira ya joto ulianza leo na utaendelea hadi Agosti 31, 2025.

Kwa mujibu wa idara kuu ya masuala ya Qur'ani ya vituo vinavyohusiana na Al-Azhar, washiriki watafundishwa kuhifadhi Qur'ani bila malipo kupitia mbinu mbili.

Mbinu ya kwanza inaitwa “Hifadhi ulichoainishiwa”, inayotekelezwa katika vituo vya Al-Azhar siku tatu kwa wiki kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 6 adhuhuri.

Mbinu ya pili inaitwa “Duru 10,000 za Qur'ani”, inayotekelezwa katika vituo binafsi vya kuhifadhi Qur'ani vinavyofanya kazi chini ya usimamizi wa Al-Azhar.

Mpango huu wa Qur'ani wa majira ya joto unatekelezwa kwa msaada wa Mkuu wa Al-Azhar, Sheikh Ahmed Al-Tayeb.

Mkurugenzi Mkuu wa Vituo Vinavyohusiana na Al-Azhar pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Masuala ya Qur'ani wa Al-Azhar watausimamia mpango huu.

3493292

Habari zinazohusiana
Kishikizo: al azhar qurani tukufu
captcha