iqna

IQNA

Uislamu Marekani
TEHRAN (IQNA)- Bilionea wa Kimarekani, Elon Musk, ambaye ni mmiliki wa mtandao wa kijamii wa Twitter, amewakasirisha Waislamu nchini Marekani baada ya kuchapisha picha kwenye akaunti yake ya Twitter, ikiwa na idadi ya alama za fikra na itikadi anazodai zinalenga "kupindua na kuharibu fikra na akili za watu."
Habari ID: 3476345    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/01/02

Waislamu Kanada
TEHRAN (IQNA) - Jumuiya ya Waislamu wa Kanada (MAC) itaandaa mashindano yake ya 20 ya Qur'ani Tukufu Januari Mosi 2023.
Habari ID: 3476337    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/31

Waislamu Ufaransa
TEHRAN (IQNA) – Msikiti wa Jamia wa Paris, Ufaransa unawasilisha malalamiko ya jinai dhidi ya mwandishi Mfaransa Michel Houellebecq kutokana na kauli zake dhidi ya Uislamu na Waislamu.
Habari ID: 3476330    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/30

Ibada ya Umrah
TEHRAN (IQNA) – Katika mpango uliobuniwa na mamlaka ya Saudia, Waislamu wapya 100 walitembelea Msikiti Mtakatifu wa Makka na Msikiti wa Mtume SAW mjini kutekeleza ibada ya Hija ndogo ya Umrah kwa mara ya kwanza.
Habari ID: 3476323    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/29

Waislamu Kanada
TEHRAN (IQNA) – Waislamu katika mji wa Okotoks nchini Kanada sasa wana nafasi ya Sala ya Ijumaa kufuatia ushirikiano na kanisa moja la mji huo.
Habari ID: 3476316    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/27

Waislamu Ujerumani
TEHRAN (IQNA) – Maiti ya Muislamu mmoja ilichomwa moto nchini Ujerumani baada ya hospitali mjini Hannover kuchanganya maiti mbili.
Habari ID: 3476294    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/23

Uislamu na Elimu
TEHRAN (IQNA)- TEHRAN (IQNA) – Shirika la Kiislamu la Elimu, Sayansi na Utamaduni Duniani (ISESCO) linapanga kuanzisha mfuko kwa ajili ya kusaidia wasomi na watu mahiri katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 3476288    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/22

Waislamu Kenya
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Ulinzi nchini Kenya, Aden Duale Jumanne ameunga mkono vazi la Hijabu ambapo amewataka wanokerwa na wanawake wa Kiislamu kuvaa vazi hilo la stara nchini Kenya watafute nchi nyingine ya kuishi.
Habari ID: 3476284    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/21

Uislamu unavyoenea
TEHRAN (IQNA) – Maafisa wa Kuwait wanasema jumla ya watu 109 wamesilimu nchini humo tangu mwanzoni mwa mwaka huu.
Habari ID: 3476270    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/19

Waislamu wa Kanada
TEHRAN (IQNA) - Wanachama wa Taasisi ya Misaada ya Kiislamu Kanada wametayarisha mamia ya vifurishi vya misaada maalumu ya majira ya baridi kali kwa ajili ya watu wasio na makazi wa Metro Vancouver siku ya Jumamosi.
Habari ID: 3476267    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/18

Waislamu nchini Nigeria
TEHRAN (IQNA) - Gavana wa Jimbo la Borno la Nigeria Ijumaa alitangaza ufunguzi wa mashindano ya kila mwaka ya kuhifadhi Qur'ani yaliyoandaliwa na Kituo cha Mafunzo ya Kiislamu cha Chuo Kikuu cha Usman Dan Fodio.
Habari ID: 3476259    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/17

Waislamu Uingereza
TEHRAN (IQNA)-Katika mkutano kamili wa Baraza la Serikali za Mitaa la Eneo la Scotland, la Uingereza wiki iliyopita, diwani Ali Salamati (Kilbride Magharibi Mashariki) alileta hoja ya kuitaka mamlaka ya eneo hilo azimio la kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu au Islamophobia.
Habari ID: 3476253    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/15

Uislamu nchini Ghana
TEHRAN (IQNA) – Baraza la Umoja na Maendeleo ya Waislamu limezinduliwa nchini Ghana kwa lengo la kukuza mshikamano na ustawi wa jamii ya Waislamu katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.
Habari ID: 3476250    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/14

Harakati za Qur'ani Tukufu
TEHRAN (IQNA) – Semina ya pili ya Qur’ani ya Chuo Kikuu cha Kiarabu cha Amman katika mji mkuu wa Jordan ilifanyika katika kitivo cha teolojia ya Kiislamu cha chuo hicho.
Habari ID: 3476249    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/14

Waislamu Duniani
TEHRAN (IQNA) - Wananchi Waislamu wa Nigeria wameandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo, Abuja, kulalamikia ukandamizaji dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia katika Jamhuri ya Azerbaijan.
Habari ID: 3476235    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/11

Uislamu na Waislamu
TEHRAN (IQNA)- Mwanamasumbwi wa kulipwa wa zamani wa Marekani, Mike Tyson, amefika katika mji mtakatifu wa Makka, eneo takatifu zaidi katika Uislamu, na kutekeleza ibada ya Umrah (Hija Ndogo).
Habari ID: 3476227    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/10

Waislamu Uingereza
TEHRAN (IQNA) – Waislamu kadhaa wa Uingereza wamewashutumu polisi wa nchi hiyo kwa kuwatendea vibaya kama "magaidi" wakati walipokamatwa kwa tuhuma za chuki dhidi ya Wayahudi ambazo baadaye zilitupiliwa mbali.
Habari ID: 3476220    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/09

Waislamu Ujerumani
TEHRAN (IQNA) – Visa 120 vya uhalifu wa chuki dhidi ya Uislamu viliripotiwa nchini Ujerumani katika robo ya tatu ya mwaka huu.
Habari ID: 3476213    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/07

Hali ya Waislamu Uganda
TEHRAN (IQNA)- Waislamu nchini Uganda kutoka makundi yote ya jamii jana Jumatatu walipinga kukamatwa kiholela kwa viongozi wa Waislamu wakati wa uvamizi wa misikiti.
Habari ID: 3476206    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/06

Hali ya Waislamu Nigeria
TEHRAN (IQNA) Watu wenye silaha wameshambulia msikiti mmoja kaskazini mwa Nigeria na kuwateka nyara watu 19 huku visa vya utekaji nyara vikiongezeka nchini humo.
Habari ID: 3476205    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/12/06