Jinai za Israel
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema katika chapisho la ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X jana Jumapili kwamba kukata ufadhili kwa UNRWA "kutawaumiza tu watu wa Gaza".
Habari ID: 3478278 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/30
Watetezi wa Palestina
IQNA - Mamia ya watu walikusanyika katika Kituo cha Kiislamu cha Maine siku ya Jumapili kuwaandikia barua wawakilishi wao, wakiwataka kuunga mkono takwa la kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel usitisha vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Gaza. Wapalestina wasiopungua 26,000 wameuawa shahidi tangua utawala wa Israel uanzishe vita dhidi ya Gaza Oktoba mwaka jana.
Habari ID: 3478273 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/29
Jinai za Israel
IQNA - Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi la Palestina UNRWA amesema kuwa uamuzi wa baadhi ya nchi za Magharibi kusitisha misaada ya kifedha kwa shirika hilo ni sawa na "adhabu ya pamoja" ambayo itapunguza misaada ya kuokoa maisha kwa watu milioni mbili huko Gaza.
Habari ID: 3478265 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/28
Kadhia ya Palestina
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: Nchi za Kiislamu zinapaswa kukata uhusiano wao wa kisiasa na kiuchumi na utawala wa Kizayuni kwa kukata mishipa muhimu ya uhai ya utawala huo ghasibu.
Habari ID: 3478242 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/23
Jinai za Israel
IQNA-Ripota wa Umoja wa Mataifa anasema utawala wa Kizyuni wa Israel unatumia njaa kama silaha dhidi ya watu Wapalestina wa Gaza ambao wanakabiliwa na mgogoro mkubwa wa chakula baada ya miaka ya vikwazo na vita vya sasa vya maangamizi ya umati vinavyotekelezwa na Israel.
Habari ID: 3478241 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/23
Jinai za Israel
IQNA - Wapiga kura wa Marekani wamehimizwa kuandika "Sitisha Vita Gaza" kwenye kura zao wakati wa kuchagua wagombea wa uchaguzi wa rais wa mwezi Novemba ikiwa ni njia ya kubainisha malalamiko kuhusu jinsi Joe Biden alivyoshughulikia vita vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Gaza.
Habari ID: 3478238 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/23
Jinai za Israel
IQNA-Wizara ya Wakfu na Masuala ya Dini katika Ukanda wa Gaza imesema mashambulizi ya vikosi vya utawala katili wa Israel dhidi ya eneo hilo lililozingirwa yamebomoa na kuharibu misikiti 1,000 tokea Oktoba 7 mwaka uliopita hadi sasa.
Habari ID: 3478234 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/22
Jinai za Israel
IQNA-Utawala wa Kizayuni wa Israel umewauwa maprofesa 94 wa vyuo vikuu, mamia ya walimu, na maelfu ya wanafunzi katika Ukanda wa Gaza katika muda wa miezi mitatu, kwa mujibu wa shirika moja huru la kutetea haki za binadamu.
Habari ID: 3478233 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/22
Jinai za Israel
IQNA-Serikali za Mexico na Chile zimeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kuchunguza na kuwashtaki maafisa wa utawala wa Israel ambao wamehusika katika jinai za kivita dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478215 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/19
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza katika kikao cha maimamu wa Ijumaa kote Iran kuwa: Watu madhulumu na wenye nguvu wa Ghaza wameweza kuwaathiri walimwengu kwa mapambano yao.
Habari ID: 3478205 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/16
Jinai za Israel
IQNA - Shirika la Umoja wa Mataifa la kutoa misaada ya kibinadamu (OCHA) liliripoti kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kuzuia utoaji wa misaada muhimu ya kibinaadamu ikiwa ni pamoja na dawa muhimu na mafuta ya kuendesha huduma za maji na usafi wa mazingira kaskazini mwa Gaza.
Habari ID: 3478204 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/16
Jinai za Israel
IQNA - Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu (OCHR) imesisitiza haja ya kusitishwa mara moja mapigano katika Ukanda wa Gaza ili kumaliza mauaji na mateso ya wananchi wakati vita vya utawala wa Israel dhidi ya eneo hilo vikwa vinakaribia kutimia siku 100.
Habari ID: 3478189 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/13
Watetezi wa Palestina
IQNA-Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) imeanza kusikiliza shauri la kesi iliyofunguliwa na Afrika Kusini dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel, ambayo inaishutumu kwa kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Gaza.
Habari ID: 3478184 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11
Watetezi wa Palestina
IQNA-Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amesema utawala haramu wa Israel umeshindwa kufikia malengo yake yoyote baada ya takriban siku 100 za vita vya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478183 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11
Watetezi wa Palestina
IQNA- Nchi zaidi zimeungana na Afrika Kusini katika kesi iliyowasilishwa dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu vita vya mauaji ya kimbari vya utawala huo kwenye dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
Habari ID: 3478182 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11
Watetezi wa Palestina
IQNA - Mkutano wa kimataifa umepangwa kufanyika Tehran wikendi hii kutangaza mshikamano na Wapalestina wa Ukanda wa Gaza, ambao wamekuwa chini ya mashambulizi yasiyo na kikomo ya utawala haramu Israel kwa zaidi ya miezi mitatu.
Habari ID: 3478181 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11
Jinai za Israel
IQNA-Spika wa Bunge la Iran Mohammad Baqer Qalibaf anasema utawala wa Kizyauni wa Israel uliasisiwa kwa mauaji ya kimbari na vita na hivyo kuendelea kuwepo kwake kunategemea kutekeleza jinai hizo za kutisha.
Habari ID: 3478179 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/10
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, njama kubwa za maadui ni kuwatoa uwanjani wananchi wa Iran na kwamba Ukanda wa Gaza hivi sasa ni mfano wa wazi na wa kivitendo wa nguvu kubwa za wananchi huku akisisitiza kuwa historia haitasahau jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wanawake na watoto Wapalestina.
Habari ID: 3478174 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/09
Jitihada
IQNA - Licha ya mashambulizi ya mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza ambayo yamepelekea watu ya 23,000 kupoteza maisha na malaki kuyahama makazi yao, mafunzo ya Qur'ani Tukufu yanaendelea katika eneo hilo lililozingirwa.
Habari ID: 3478163 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/07
Watetezi wa Palestina
IQNA – Makumi ya makundi na mashirika ya kijamii nchini Marekani yametangaza azma ya kushiriki katika maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika Washington, DC, kuunga mkono Wapalestina wanaodhulumiwa na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478158 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/06