ukanda wa gaza

IQNA

IQNA-Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu imetangaza Jumapili kuwa Gaza imegeuka kuwa sehemu hatari kuliko zote duniani kwa wanahabari, huku angalau wafanyakazi 295 wa vyombo vya habari wakithibitishwa kuuawa katika mashambulizi ya Israel tangu kuanza kwa vita Oktoba 2023.
Habari ID: 3482200    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/04

IQNA – Msafara wa meli unaojulikana kama Global Sumud Flotilla, unaolenga kuvunja mzingiro uliowekwa na utawala katili wa Israeli dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, umefika katika maji ya kimataifa karibu na pwani ya Ugiriki.
Habari ID: 3482179    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Wakielezea kama uhamasishaji mkubwa zaidi wa aina yake, wanaharakati wa kimataifa wametangaza mipango ya kupeleka meli 200 katika msafara wa misaada unaojulikana kama Freedom and Sumud Flotilla, wakilenga Ukanda wa Gaza katika majira ya kuchipua mwaka huu.
Habari ID: 3482002    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/27

IQNA-Kiongozi wa harakati ya Muqawama (mapambano ya Kiislamu) ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa Marekani na Utawala wa Israel zinakabiliana na Iran kwa sababu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasimama kama kizuizi dhidi ya mradi wao mpana wa kutawala eneo la Asia Magharibi au Mashariki ya Kati.
Habari ID: 3481932    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/14

IQNA – Hafla maalumu imefanyika Gaza kuadhimisha mahafali ya wanafunzi kadhaa wa kike waliokamilisha kuhifadhi Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3481738    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/30

IQNA – Sherehe imefanyika katika Kambi ya Wakimbizi ya Al-Shati, magharibi mwa Gaza, kuadhimisha wanaume na wanawake 500 waliokamilisha kuhifadhi Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3481722    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/27

IQNA-Wakipita njia zilizozungukwa na majengo yaliyoharibiwa na vifusi, wanafunzi Wapalestina wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Gaza wiki hii wamerudi darasani kwa mara ya kwanza baada ya miaka miwili.
Habari ID: 3481692    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/21

IQNA – Dar al-Ifta ya Misri imetoa fatwa mpya ya kidini inayoruhusu raia kuelekeza mali ya zakat kusaidia mahitaji ya msingi ya watu waliokoseshwa makazi huko Gaza.
Habari ID: 3481373    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/15

IQNA – Kijana mmoja wa Kipalestina amegundua nakala ya Msahafu ikiwa salama kabisa chini ya magofu ya nyumba yake iliyoharibiwa kaskazini mwa Gaza, akieleza hisia za kina na shukrani baada ya miezi ya mashambulizi.
Habari ID: 3481371    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/15

IQNA – Baada ya miezi kadhaa ya kufungwa kutokana na mashambulizi ya angani, Msikiti wa Al-Tawhid ulioko katika kambi ya wakimbizi ya Al-Shati, Gaza, umefunguliwa tena na sauti ya adhana imeanza kusikika kwa mara nyingine.
Habari ID: 3481366    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/14

IQNA – Sherehe ya watu wa Gaza kwa ajili ya kusitishwa kwa vita ni yao pekee, si ya Donald Trump, ambaye ametangaza kuwa atatembelea eneo hilo kuchukua sifa kwa kile anachokiita “tukio la kihistoria”.
Habari ID: 3481349    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/10

IQNA-Vita vya Ghaza na jinai nyingine zinazofanywa na utawala ghasibu wa Israel zimekabiliwa na msururu wa mashinikizo ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni ambayo yameufanya utawala huo ghasibu kuwa taifa linalochukiwa na kukataliwa duniani.
Habari ID: 3481334    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/05

IQNA – Idadi kubwa ya watu wameshiriki katika maandamano katika nchi mbalimbali kuonyesha mshikamano na Gaza na kulaani hatua ya Israel kuuteka nyara Msafara wa Meli wa Global Sumud uliokuwa umebeba misaada ya kibinadamu kuelekea eneo hilo a Wapalestina.
Habari ID: 3481319    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/03

IQNA – Hatua ya utawala wa Israeli kuzuia meli za Msafara wa Kimataifa wa Sumud imezua shutuma kali kutoka kwa serikali na mashirika ya kimataifa kote duniani.
Habari ID: 3481315    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/02

IQNA – Harakati za mapambano ya ukombozi wa Wapalestina, Hamas na Jihad ya Kiislamu, zimetoa matamko ya kulaani hatua ya Marekani kutumia kura ya turufu au veto kuzuia kupitishwa kwa rasimu ya azimio la kusitisha vita Gaza, wakisema kuwa hatua hiyo inachochea jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3481253    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/19

IQNA – Washiriki wa mkutano wa kimataifa wa wanawake uliofanyika Tehran wametoa wito wa kususiwa kwa kina kwa utawala wa Kizayuni, wakilaani vita vya mauaji ya halaiki vinavyoendelea dhidi ya Gaza.
Habari ID: 3481210    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/09

IQNA – Akielezea unyama unaoendelea kufanywa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina, Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amesisitiza haja ya kukatisha mahusiano yote na Israel.
Habari ID: 3481187    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/05

IQNA- Maandamano yafanyika Uingereza kulaani  mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel dhidi ya Gaza Maandamano makubwa yamefanyika nje ya ubalozi wa utawala wa Israel mjini London, Uingereza kulaani mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3481127    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/24

IQNA-Kiongozi mkuu Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatullah Sayyid Ali al-Sistani, ameelezea masikitiko yake makubwa kuhusu hali ya kibinadamu inayoendelea kuzorota katika Ukanda wa Gaza, hususan baa la njaa linalozidi kushika kasi, na kutoa wito kwa mataifa ya Kiarabu na Kiislamu kuchukua hatua za haraka kukomesha janga hili la kusikitisha.
Habari ID: 3481002    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/26

IQNA – Mwanazuoni wa ngazi za juu wa Kiislamu kutoka Iran amewataka viongozi wa Kiislamu na Kiongozi wa Kanisa Katoliki kushikamana dhidi ya mzingiro wa Israel huko Gaza, ambako njaa inazidi kupelekea janga kubwa la kibinadamu.
Habari ID: 3480992    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/24