iqna

IQNA

Waislamu Uingereza
IQNA - Mwanamume mmoja amerekodiwa kwenye video akirusha maneno ya chuki dhidi ya Uislamu na kumtemea mate dereva wa basi Muislamu mjini London huku kukiwa na ongezeko la ghasia dhidi ya Waislamu katika nchi hiyo ya Ulaya.
Habari ID: 3479249    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/09

Machafuko Uingereza
IQNA: Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uingereza, Yvette Cooper, siku ya Jumatatu alibainisha chuki dhidi ya Uislamu kama kichocheo cha ghasia za hivi karibuni za wazungu wenye misimamo mikali wa mrengo wa kulia katika miji kadhaa, ambayo imesababisha uharibifu mkubwa na karibu watu 400 kukamatwa.
Habari ID: 3479237    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/06

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA – Tukio la Muislamu kudungwa kisu katika kituo cha treni cha Blundellsands & Crosby huko Liverpool limeacha jamii ya Waislamu wa jiji hilo katika mshtuko huku Waislamu kote Uingereza sasa wanahofia usalama wao huku kukiwa na maandamano ya magenge ya watu wenye misimamo mikali ya chuki ya mrengo wa kulia.
Habari ID: 3479222    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/03

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA - Vichwa vitatu vya nguruwe vimepatikana nje ya shule mbili na kituo cha vijana huko Rainham, Uingereza vikiambatana na maandishi ya chuki dhidi Uislamu.
Habari ID: 3479192    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/27

Waislamu Ujerumani
IQNA - Shirika moja lisilo la kiserikali la kimataifa lenye makao yake makuu nchini Iran limelaani vikali marufuku ya Ujerumani dhidi ya Kituo cha Kiislamu cha Hamburg (IZH) na kuitaja hatua hiyo kama ukiukaji wa wazi wa mikataba ya kimataifa, pamoja na haki za binadamu na uhuru wa dini, kujieleza na kukusanyika.
Habari ID: 3479191    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/27

Waislamu Ujerumani
IQNA- Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Ali Bagheri Kani amelaani vikali hatua ya polisi ya Ujerumani ya kupiga marufuku Kituo cha Kiislamu cha Hamburg (IZH) na asasi zake tanzu, na kusema kwamba hatua hiyo inakiuka kanuni za kimsingi za uhuru wa kuabudu.
Habari ID: 3479189    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/26

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA – Matukio ya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) yaliongezeka nchini Luxembourg mwaka jana, kulingana na utafiti uliofanywa na Luxembourg Observatoire de L'Islamophobie.
Habari ID: 3479181    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/25

chuki dhidi ya Waislamu nchini Ujerumani
Umoja wa Uturuki na Kiislamu kwa Masuala ya Kidini (DİTİB) umeelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya kuongezeka kwa visa vya chuki dhidi ya Waislamu nchini Ujerumani.
Habari ID: 3479089    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/08

Chuki Dhidi ya Uislamu Marekani
Mwanamke mmoja Kaskazini mwa Texas amekamatwa tena na anakabiliwa na dhamana ya dola milioni moja baada ya kushtakiwa kwa jaribio la kuua watoto wawili wa Kiislamu.
Habari ID: 3479057    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/03

Wito wa chuki’
Kundi la kutetea haki za Waislamu nchini Marekani limekashifu matamshi ya mjumbe wa Israel dhidi ya Waislamu, na kubainisha kwamba kauli kama hizo zitaongeza chuki na unyanyasaji dhidi ya Waislamu mjini New York.
Habari ID: 3479041    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/01

Ujerumani Chuki Dhidi ya Uislamu
Kulingana na shirika lisilo la kiserikali nchini Ujerumani, chuki dhidi ya Uislamu imeongezeka kwa asilimia 140 mwaka huu katika nchi hiyo.
Habari ID: 3479019    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/27

Chuki dhidi ya Uislamu India
Watu walizuia Shirika la Manispaa ya Delhi (MCD) kubomoa ukuta wa mpaka wa msikiti katika wilaya ya Rohini siku ya Jumanne.
Habari ID: 3479016    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/27

Kadhia ya Palestina
Mama Muislamu na watoto wake walikua wahasiriwa wa madai ya jaribio la mauaji katika kidimbwi cha kuogelea cha ghorofa huko Euless, Texas.
Habari ID: 3478999    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/22

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA - Tume ya Baraza la Ulaya ya Kupinga Ubaguzi wa Rangi (ECRI) imetoa ripoti yake ya kila mwaka, ikifichua mwelekeo unaohusiana wa kuongezeka kwa ubaguzi dhidi ya wagonjwa Waislamu wanaotafuta huduma za afya Ulaya.
Habari ID: 3478996    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/21

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA-Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani (CAIR) eneo la San Francisco Bay Area (CAIR-SFBA) limelaani vikali mashambulizi ya maneno ya chuki yaliyolenga jamii ya Waislamu wakati wa Eid Al-Adha.
Habari ID: 3478992    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/20

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA - Baraza la Kitaifa la Waislamu wa Canada (NCCM) limeripoti kuongezeka kwa 1300% kwa matukio ya chuki dhidi  ya Uislamu (Islamophobia) katika nchi hiyo ya Amerika Kaskazini kufuatia kuanza kwa mauaji ya kimbari ya Isarel dhidi ya Wapalestina huko  huko Gaza.
Habari ID: 3478943    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/07

Waislamu Ufaransa
IQNA - Msikiti Mkuu wa Paris ulimkosoa waziri mkuu wa Ufaransa kwa matamshi yake ya hivi karibuni ya chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3478751    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/04/30

Waislamu Marekani
IQNA – Ofisi ya Maadili ya  Chuo Kikuu cha Duke nchini Marekani imeanzisha uchunguzi kuhusu uchafuzi wa mabango kuhusu mwezi wa Ramadhani,  jambo ambalo limeibua wasiwasi wa chuki dhidi ya Uislamu ndani ya a chuo hicho.
Habari ID: 3478750    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/04/30

Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA - Inaonekana hakuna nia nchini Uswidi ya kukomesha vitendo vya kuvunjia heshima Qur'ani Tukufu, vitendo ambavyo vimewasikitisha na kuwakasirisha Waislamu kote ulimwenguni.  
Habari ID: 3478747    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/04/28

IQNA-Wanafunzi wa aislamu katika Chuo Kikuu cha Rutgers nchini Marekani wameelezea wasiwasi juu ya usalama wao baada ya kituo chao cha Kiisilamu kuharibiwa wakati wa siku kuu ya Idul Fitr.
Habari ID: 3478675    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/04/12