Kamati ya Sera za Kigeni katika Umoja wa Ulaya imetangaza vikwazo vipya dhidi ya utawala wa Israel kutokana na hatua za utawala huo za kuvuruga usalama wa Baitul Maqdis na kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Habari ID: 1475311 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/19
Mabunge ya Uhispania na Ufaransa yamepanga kupigia kura azimio la kulitambua taifa la Palestina, hatua ambayo imekuwa ikichukuliwa ma nchi kadhaa za Ulaya.
Habari ID: 1473023 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/14
Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa, kumeundwa kamati ya uchunguzi kuhusiana na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel katika ukanda wa Gaza.
Habari ID: 1472788 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/13
Kufuatia kuongezeka na kuenea malalamiko ya Wa palestina katika mji wa Quds (Baitul Maqdis) unaokaliwa kwa mabavu, Ghaza na Ukingo wa Magharibi hivi sasa Wa palestina wanaoishi katika Palestina inayokaliwa kwa mabavu, yaani Israel, nao pia wameandamana.
Habari ID: 1471813 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/10
Ghasia na machafuko mapya yamezuka kati ya askari wa utawala wa kizayuni wa Israel na waandamanaji wa Palestina katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na Israel baada ya utawala huo kufunga Msikiti mtukufu wa al Aqsa.
Habari ID: 1470536 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/06
Sheikh Bilal Shaaban Katibu Mkuu wa chama cha Hizb Tauhid Islami nchini Lebanon amejiunga na wapenda uhuru na haki duniani katika kulaani vikali hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel kufunga milango ya Msikiti wa Al Aqsa na kuwazuia Waislamu kuswali ndani ya msikiti huo.
Habari ID: 1466340 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/01
Utawala haramu wa Kizayuni, kwa mara ya kwanza leo Ijumaa alfajiri umefungua milango ya Msikiti wa al-Aqsa baada ya kuifunga mwaka 1967. Utawala huo pia umeshadidisha ulinzi katika maeneo ya jirani na msikiti huo, kutokana na hofu ya kuzuka mapambano makali kutoka kwa Wa palestina .
Habari ID: 1465817 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/31
Imam Khamenei
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa ushindi wa Ghaza wa mapambano katika vita vya siku 50 na matamshi ya kushindwa utawala wa Kizayuni mbele ya raia waliozingirwa ni ushindi mkubwa na dhihirisho la ahadi na msaada wa Mwenyezi Mungu na ni bishara ya kufikia ushindi mkubwa zaidi.
Habari ID: 1460936 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/17
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imetaka washtakiwe wakuu wa kijeshi na kisiasa wa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kutenda jinai dhidi ya binadamu.
Habari ID: 1455018 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/28
Ali Larijani
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu yaani bunge la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inataka kuimarisha umoja, udugu na mwamko wa Kiislamu katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 1448576 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/09
Ayatullah Mohsen Araqi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu ya Kiislamu Ayatullah Mohsen Araqi ameashiria ufanisi wa mapambano ya watu wa Palestina mbele ya hujuma ya utawala wa Kizayuni katika vita vya hivi karibuni vya Ghaza.
Habari ID: 1448558 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/09
Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Isalmi ya Palestina
Ramadhan Abdullah Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina amesema utawala wa Kizayuni wa Israel ulipata pigo la kistratijia hivi akribuni katika vita vyake vya siku 51 dhidi ya Wa palestina katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 1448553 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/09
Ali Larijani
Ali Larijani Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran yaani Bunge amesema , leo taifa la Iran linafakhari kuwa, kwa uwezo wake wote limeweza kulisaidia taifa la Palestina katika kipindi chake kigumu zaidi.
Habari ID: 1443997 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/28
Maelfu ya Wa palestina katika Ukanda wa Gaza wameendelea kusherehekea kufikiwa makubaliano ya muda mrefu kuhusu usitishaji mapigano kati ya makundi ya muqawama na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 1443936 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/27
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitaka jamii ya kimataifa na hususan mashirika ya misaada ya kibinadamu kuushinikiza utawala wa Kizayuni uache kuuzingira Ukanda wa Ghaza na uruhusu misaada ya kibinadamu iwafikie wakazi wa ukanda huo uliozingirwa kila upande.
Habari ID: 1440685 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/18
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amesema utawala wa Kizayuni wa Israel unapaswa kulipa fidia ya jinai zake huko Ghaza kwa kuondoa mzingiro dhidi ya Wa palestina katika ukanda huo wa pwani.
Habari ID: 1439233 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/14
Rais Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Waislamu katika Ukanda wa Ghaza hatimaye watapata ushindi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel na kwamba Iran daima itasimama pamoja mataifa yote yanayodhulimiwa wakiwemo Wa palestina , Wairaqi na Wasyria.
Habari ID: 1436787 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/06
Makubaliano ya muda ya usitishwaji vita yameanza kutekelezwa katika Ukanda wa Ghaza baada ya utawala ghasibu wa Israel kulazimika kukubali masharti ya wanamapambano wa Ki palestina ya kuondoa majeshi yake katika ukanda huo.
Habari ID: 1436767 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/06
Jeshi la utawala haramu wa Israel limeendeleza mauaji ya umati katika eneo la Ukanda wa Ghaza hii leo kwa siku ya 28 mtawalia na kuifanya idadi ya mashahidi wa hujuma hiyo kukaribia 2,000.
Habari ID: 1435964 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/04
Rais Hassan Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuendelea kimya na kutojali Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa UNSC ndio chanzo kikuu ambacho kimeufanya utawala wa Kizayuni wa Israel uendelee kupata kiburi cha kuendeleza jinai zake dhidi ya Wa palestina katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 1435944 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/04