kiislamu - Ukurasa 16

IQNA

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu ya Kiislamu amewataka Waislamu kuwa macho katika kukabiliana na njama za maadui wa ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 2689576    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/09

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema madola ya kibeberu yanaibua migogoro baina ya Waislamu kwa lengo la kutawala ardhi za Kiislamu zenye umuhimu wa kistratijia.
Habari ID: 2684305    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/07

Mkutano wa 28 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu umeanza leo mjini Tehran kwa kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu na maulamaa wa ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 2684304    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/07

TEHRAN-IQNA- Mashindano ya 5 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Wanachuo Waislamu yamemalizika Jumapili mjini Tehran huku wawakilishi wa Iran na misri wakichukua nafasi za kwanza katika qiraa na hifdhi kwa taratibu.../mh 2671946
Habari ID: 2672141    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/05

Mwenyekiti wa Taasisi ya Jihadi ya Vyuo Vikuu nchini Iran amesema lengo la Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani ya Wanachuo Waislamu ni kuimarisha itikadi za wanafunzi wa vyuo vikuu katika ulimwengu wa Kiislamu ili kuhuisha umoja wa Waislamu kueneza ustaarabu mpya wa Kiislamu.
Habari ID: 2666237    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/01

Kikao cha 23 kikuu cha Sala nchini Iran kimefunguliwa Jumatano kwa ujumbe wa Ayatullah Udhma Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu mjini Ahwaz (kusini magharibi mwa Iran).
Habari ID: 2663165    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/01

Kiongozi mwandamizi wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Uganda Sheikh Ductoor Abdul Qadir Sudi Muwaya aliuawa shahidi Alkhamisi iliyopita. Mkuu wa polisi nchini humo ametangaza kuwa uchunguzi wa kina utafanyika kubainisha aliyetekeleza mauaji hayo.
Habari ID: 2646978    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/29

Tehran (IQNA)- Kongamano la kimataifa lenye anuani ya “Umoja wa Kimataifa Kwa Mtazamo wa Qur’ani na Hadithi” linatazamiwa kufanyika Tehran, Ijumaa tarehe pili Januari.
Habari ID: 2626656    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/25

Tumo katika kumbukumbu ya kufariki dunia Mtume wa mwisho wa Mwenyezi Mungu Muhammad al-Mustafa SAW. Hii leo imepita zaidi ya miaka 1400 tangu mbora huyo wa viumbe aage dunia; lakini jina la mtukufu huyo pamoja na utajo na shakhsia yake kubwa na adhimu na isiyo na mithili ingali inaleta hamasa katika nyoyo.
Habari ID: 2623557    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/20

Kituo cha Kiislamu cha al Azhar nchini Misri kimetoa wito wa kufukuzwa magaidi wote katika nchi za Waislamu.
Habari ID: 2617813    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/12

Mjumbe maalumu wa rais Vladimir Putin wa Russia amekutana na kufanya mazungumzo na katibu mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon.
Habari ID: 2615883    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/07

Kiongozi wa Jumuiya ya Jamaatud Dawa nchini Pakistna Hafidh Saeed Ahmad ametoa wito wa kuanzishwa 'Umoja wa Mataifa ya Kiislamu' ili kutatua matatizo waliyonayo Waislamu duniani.
Habari ID: 2615835    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/07

Mkutano wa 10 wa Mawaziri wa Habari wa nchi za Kiislamu (ICIM) umefanyika Jumatano hapa mjini Tehran kwa kuhudhuriwa na Is’haq Jahangiri Makamu wa Kwanza wa Rais na Katibu Mkuu wa OIC.
Habari ID: 2615009    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/04

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ege kilichoko katika mji wa Izmir nchini Uturuki amehukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka miwili jela, baada ya kumzuia mwanafunzi aliyevaa hijabu ya Kiislamu kuingia darasani.
Habari ID: 2613249    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/30

Imam Khamenei
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, kujihisi kuwa na majukumu ya kibinadamu, kuwa na maarifa ya kumjua Mwenyezi Mungu na busuri, ni misingi mikuu ya fikra za kimantiki za jeshi la kujitolea la Basiji.
Habari ID: 2612444    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/28

Kongamano la Kimataifa kuhusiana na Tishio la Makundi ya Kitakfiri na Yenye Kufurutu Ada limeanza leo katika mji mtukufu wa Qum hapa nchini Iran kwa kuhudhuriwa na masheikh na maulamaa kutoka nchi mbalimbali duniani.
Habari ID: 1476323    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/23

Imam Khamenei
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametahadharisha kuhusu njama za adui zenye lengo za kuudhihirisha Uislamu kuwa ni tishio.
Habari ID: 1474768    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/18

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amemteua Dakta Muhammad Sarafraz kuwa Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB) kwa kipindi cha miaka mitano.
Habari ID: 1471116    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/08

Ghasia na machafuko mapya yamezuka kati ya askari wa utawala wa kizayuni wa Israel na waandamanaji wa Palestina katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na Israel baada ya utawala huo kufunga Msikiti mtukufu wa al Aqsa.
Habari ID: 1470536    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/06

Imam Khamenei
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei, amesema kuwa, ibada ya hija ni fursa bora kabisa kwa ajili ya kukabiliana na njama za kuitenganisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na ulimwengu wa Kiislamu na nara yake ya ‘kukabiliana na shubha na propaganda zinazoenezwa na maadui wa Uislamu’ na kutoa jibu mwafaka kwa mahitaji ya kimaanawi na kifikra za mahujaji.
Habari ID: 1465135    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/28