iran - Ukurasa 2

IQNA

IQNA – Zaidi ya watu 67,000 wamejisajili kwa ajili ya duru ya 49 ya Mashindano ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Muda wa mwisho wa usajili, ambao ulikuwa umeongezwa mara moja, umefika tamati siku ya Jumatatu.
Habari ID: 3482289   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/27

IQNA-Katika ujumbe wake kwa mnasaba wa kuwadia msimu wa Hijja ya Nabii Ibrahim (as), Ayatullah Seyyed Mojtaba Hosseini Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, ametaja amali na thikri zilizajaa maana za Hijja na kusema ni ishara za kudumu milele kwa wanadamu kwa ajili ya kuwahamasisha waelekee kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Habari ID: 3482288   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/26

IQNA – Kwa kuwasili kwa kundi la mwisho la Wairni mjini Madina kwa ajili ya Hija ya mwaka 1447 (2026), mchakato wa kuwasafirisha waumini kuelekea Ardhi ya Wahyi umekamilika. Zaidi ya waumini 30,000 wamesafiri kutoka nchini humo kwenda Ardhi ya Wahyi kupitia safari za ndege 130 kwa ajili ya Ibada ya Hija mwaka huu.
Habari ID: 3482262   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/20

IQNA – Rais wa Iran Masoud Pezeshkian katika ujumbe wake kwa Papa Leo XIV ameshukuru misimamo ya kimaadili ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki kuhusu mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, akiyataja kuwa ni ukiukaji wa utawala wa sheria na wa maadili ya kibinadamu.
Habari ID: 3482246   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16

Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa
IQNA-Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa kimesema kuwa ushiriki, uwezeshaji na ushirikiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika vita vya hivi karibuni vya uchokozi vilivyoanzishwa na Marekani pamoja na utawala wa Israel dhidi ya Iran ni sawa na “kusaidia kambi ya ukafiri dhidi ya ndugu Waislamu” na kwa hivyo ni “haramu kabisa.”
Habari ID: 3482238   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/14

IQNA – Papa Leo XIV amemtunuku Hujjatul‑Islam Mohammad Hossein Mokhtari, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Vatican, nishani ya juu zaidi ya kidiplomasia ya Vatican.
Habari ID: 3482235   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13

IQNA – Mufti Mkuu wa Oman ametoa wito kwa Waislamu kusimama kwa umoja katika kukabiliana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi za Kiislamu.
Habari ID: 3482224   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/10

Rais wa Iran katika Mazungumzo ya Simu na Rais wa Ufaransa:
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemwambia mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuwa Tehran iko tayari kuendelea kwa dhati kupitia njia za kidiplomasia ili kukomesha vita, huku ikisisitiza umuhimu wa kulindwa kwa haki za taifa la Iran.
Habari ID: 3482213   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/07

IQNA – Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitaka serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kusitisha kujipanga upande mmoja na kushirikiana na pande zinazoiwekea uadui Jamhuri ya Kiislamu.
Habari ID: 3482210   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/07

IQNA – Wakati mchakato wa kuwasafirisha waumini wa Iran kuelekea Saudi Arabia kwa ajili ya kutekeleza ibada ya Hija ukiendelea kushika kasi, idadi kubwa ya visa za Hija kwa waumini hao tayari zimetolewa.
Habari ID: 3482208   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/06

IQNA – Afisa wa Hija kutoka Iran ametangaza kuwasili kwa zaidi ya waumini 6,500 wa Kiirani mjini Madina kwa ajili ya kutekeleza Ibada ya Hija kufikia mwisho wa usiku wa Ijumaa.
Habari ID: 3482196   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/03

IQNA – Msomaji mashuhuri wa Qur’ani Tukufu kutoka Iraq amelaani vikali misimamo ya hivi karibuni ya qari wa Kuwait, Mishary Rashid Al Afasi, inayounga mkono dhulma ya Wamarekani na Wazayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482190   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/02

IQNA – Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Russia (Urusi) amewasilisha ujumbe wa shukrani kutoka kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, kwa Mwenyekiti wa Baraza la Mufti wa Shirikisho la Russia.
Habari ID: 3482187   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/01

IQNA – Mtaalamu wa Qur’ani Tukufu kutoka Lebanon amekosoa misimamo ya qari mmoja kutoka Kuwait akisema kuwa haina uhusiano na mafundisho ya Qur’ani.
Habari ID: 3482177   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Akikosoa kwa ukali misimamo ya qari wa Kuwait, Mishary Rashid al‑Afasi, katika kuhalalisha mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, msomaji wa Qur’ani kutoka Yemen ametoa wito wa kususiwa kwa al‑Afasi.
Habari ID: 3482173   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/28

IQNA – Katika barua mpya aliyoandika kwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Leo wa Kumi na Nne, Mkuu wa Kitengo cha Masomo ya Kiislamu katika Akademia ya Sayansi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa shukrani kwa msimamo wake wa haki katika kukataa mienendo ya ukatili.
Habari ID: 3482172   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/28

IQNA – Sheikh Osama Karbalayi, msomaji wa kimataifa wa Qur’ani kutoka Iraq, amesisitiza kuwa misimamo ya qari wa Kuwait, Mishary Rashid Al‑Afasi, katika kuhalalisha uchokozi wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, inapingana na kiini cha mafundisho ya Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3482164   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/26

IQNA – Msafara wa kwanza wa Wairani wanaoshiriki katika Ibada ya Hija mwaka huu umewasili Saudi Arabia.
Habari ID: 3482163   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/25

IQNA – Msomaji mashuhuri wa Ibtihal kutoka Misri na jaji wa mashindano ya Qur’ani ametangaza kuwa atatayarisha kasida yenye maudhui ya Qur’ani ili kukabiliana na mashambulizi ya yaliyofanywa na qari mmoja kutoka Kuwait dhidi ya Iran na mhimili wa muqawama.
Habari ID: 3482162   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/25

IQNA-Rais wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kusimama upande wa amani, utulivu na mahusiano ya kindugu katika eneo, akibainisha kwamba usalama wa eneo unapaswa kuhakikishwa na mataifa ya eneo hilo yenyewe.
Habari ID: 3482145   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/17