Masoumeh Farzaneh, mshauri wa Shirika la Awqaf la Iran amemwambia mwandishi wa IQNA kuwa wanaharakati 21 wa Qur'ani kutoka Iran na nchi kadhaa wataenziwa katika kikao hicho.
Ameongeza kuwa wanawake 450, wakiwemo 150 kutoka nchi 80, waliwasilisah kazi zao katika kongamano hilo kuhusu harakati zao Qur'ani.
Farzaneh ameongeza kuwa, makongamano yaliyopita yalisaidia kuleta maingiliano mazuri baina ya wanawake wanaharakati wa Qur'ani nchini Iran na maeneo mengine ya Waislamu duniani.
Awamu ya 33 ya Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran inaanza Jumatano hii kwa muda wa wiki moja chini ya kauli mbiu ya "Kitabu Kimoja, Ummah Moja".