Akijibu swali la tovuti ya Kuwait ya al-Anba kuhusu ulazima wa kukurubisha Waislamu wanaofuata madhehebu za Shia na Sunni, Sheikh el Tayyib alisisitiza kuwa hakuna tafauti baina ya Shia na Sunni kwani wote wanaamini kuhusu Tauhidi na Unabii wa Muhammad SAW.
Ameongeza kuwa Al Azhar inafuatilia suala la kukurubisha Waislamu wa madhehebu ya Shia na Sunni kama stratijia yake muhimu.
Sheikhe mkuu wa al Azhar pia amewakosoa wale ambao wanalenga kuibua hitilafu na migongano baina ya Waislamu wa madhehebu ya Shia na Sunni na kubainisha masikitiko yake kuwa watu hawa hawataki kuzima moto wa fitina za kimadhehebu.