Kwa mujibu wa taarifa, Gavana wa Jimbo la Kano Abdullah Gandujeh amesema imamu huyo alikiuka amri ya serikali ya kusitisha kwa muda swala za jamaa ili kuzuia kuenea corona au COVID-19.
Gavana hiyo amesema mijimuiko yote, ikiwemo ya kidini, imepigwa marufuku wakati wa kipindi hiki cha ugonjwa wa COVID-19.
Hadi kufikia Aprili 21, watu 665 walikuwa wameambukizwa corona Nigeria huku 22 miongoni mwao wakipoteza maisha.