Katika qiraa hiyo anasoma aya za Surah al Shams katika Qur’ani Tukufu. Anwar Shahat Anwar ni mwanae marhum Sheikh Muhammad Shahat Anwar na alizwaliwa mwaka 1979.
Alifanikiwa kuhifadhi Qur'ani Tukufu kikamilifu akiwa na umri wa miaka 12 kutoka kwa baba yake. Ameweza kuibuka mshindi katika mashindano mengi ya Qur'ani ya kitaifa na kimataifa. Sheikh Mahmod Shahat Muhammad Anwar amewahi kusafiri katika nchi nyingi duniani kushiriki katika mashindano ya Qur'ani.