Kituo hicho kilikuwa cha kwanza cha aina yake ambacho kilijengwa kwa ajili ya jamii inayoongozeka ya Waislamu mjini humo.
Usanifu majengo wake umeinga usanifu majengo wa Kiislamu katika zama hizi.
Kituo hicho kina msikiti wenye mnara na kubaa. Ujenzi wake ulianza mwaka 1987 na kukamilika mwaka 1991 na gharama jumla ya mradi huo ilikuwa ni dola milioni 14. Ukumbi wa Sala wa msikiti huo unaweza kubeba waumini 1,000.