IQNA

Waislamu Marekani

Marekani. Aliyehusika katika hujuma dhidi ya Msikiti akamatwa

16:48 - July 23, 2024
Habari ID: 3479174
IQNA - Mwanaume mmoja katika jimbo la Carolina Kaskazini nchini Markani amekamatwa na kushtakiwa kwa kuvamia na kuharibu msikiti Jumapili jioni.

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, tukio hilo lilitokea mwendo wa saa 5:40 usiku. katika Jumuiya ya Kiislamu ya Gastonia, iliyoko katika mtaa wa 4000 wa Barabara ya Titman.

Uharibifu wa madirisha matatu unakadiriwa kusababisha hasara ya dola 900. Nathan Reynolds Webster, 32, alikamatwa na kushtakiwa kwa uharibifu wa mali.

Tovuti ya Ofisi ya Polisi ya Gaston inaonyesha kuwa aliachiliwa muda mfupi baada ya kufungwa jela, akiwa na dhamana ya dola 1,000. Uharibifu huo unakuja huku kukiwa na ongezeko la uhalifu wa chuki dhidi ya Waislamu nchini Marekani, hasa tangu Oktoba mwaka jana wakati utawala wa Israel ulipanzisha mauaji ya kimbari dhidi ya Palestina.

3489220

Habari zinazohusiana
Kishikizo: waislamu marekani
captcha