IQNA

Muqawama (Mapambano)

Operesheni ya kihistoria ya "Kimbunga cha Al-Aqsa" ya Hamas yaangmiza Wazayuni wengi

19:51 - October 07, 2023
Habari ID: 3477698
TEHRAN (IQNA)- Wapigania ukombozi wa Palestina leo wametekeleza operesheni kubwa zaidi na ya kihistoria dhidi ya utawala dhalimu na wa kikoloni wa Israel ambapo idadi kubwa ya wanajeshi wa Kizazyuni na walowezi wa Kizayuni wameangamizwa.

Video zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinawaonyesha wanamapambano wa Muqawama wakiwa ndani ya kambi ya kijeshi leo, huku miili ya wanajeshi wa Kizayuni walioangamizwa ikiwa imezagaa huku na kule.
Takriban Waisraeli  250 wameuawa na zaidi ya 1000 kujeruhiwa, vyombo vya habari vya Israel viliripoti.
Gazeti la Times of Israel limesema wapiganaji wa Kipalestina walijipenyeza katika mji wa Sderot na makazi mengine.
 
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu Palestina, Hamas, ilitoa video inayoonyesha wapiganaji wake wamewakamata Waisraeli watatu.
 
"Vikosi vya Brigedi za Izzudin Al-Qassam (tawi la kijeshi la Hamas) vimewakamata wanajeshi kadhaa wa maadui katika vita vya Kimbunga cha  Al-Aqsa," ilisema taarifa ya Hamas.
 
Mashambulizi hayo ambayo hayajawahi kutokea yalianza dakika chache kabla ya saa 7 asubuhi wakati Waisraeli walipokuwa wakisherehekea siku ya mwisho ya tamasha la wiki la Sukkot, huku mamia ya makombora yakirushiwa yakivurumishwa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ambazo zimepachikwa jina bandia a Israel.

Tawi la kijeshi la Hamas  limesema zaidi ya makombora 7,000 yamerushwa kutoka Ukanda wa Gaza mapema leo kuelekea ardhi zinazokaliwa kwa mabavu, na kutangaza kuwa limeanzisha "Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa".

"Tumeamua kukomesha uhalifu na jinai zote za maghasibu. Wakati wao wa kufanya fujo na kujifaragua bila ya kuwajibishwa umekwisha," imesisitiza taarifa hiyo ya Izzuddin al Qassam.

Wakati huouo Harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina imetangaza kuwa wapiganaji wake wamejiunga na operesheni hiyo ya Kimbunga cha Al-Aqsa huku Hamas ikitoa wito kwa Wapalestina kila mahali walipo kujiunga na mapambano na kuyataka makundi ya Muqawama nchini Lebanon pia kujiunga na vita dhidi ya Israel.

"Sisi ni sehemu ya vita hivi, wapiganaji wetu wako bega kwa bega na ndugu zao katika Brigedi za Qassam hadi ushindi upatikane," ameeleza Abu Hamza, msemaji wa tawi la kijeshi la Jihadul-Islami kupitia mtandao wa kijamii wa Telegram.

/3485461
Habari zinazohusiana
captcha