IQNA

Jinai za Israel

Kamanda IRGC: Israel isubiri jibu kwa kumwaga damu za wasio na hatia

10:40 - June 07, 2024
Habari ID: 3478941
IQNA-Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ametahadharisha kuwa, Israel inapasa kusubiri jibu la Iran kwa kumuua shahidi mmoja wa washauri wa kijeshi wa Jamhuri ya Kiislamu katika uvamizi wa utawala huo wa Kizayuni katika mji wa Aleppo (Halab) huko kaskazini magharibi mwa Syria.

Meja Jenerali Hossein Salami, Kamanda Mkuu wa IRGC alitoa onyo hilo  Jumatano, siku mbili baada ya jeshi la utawala haramu wa Israel kufanya mashambulizi ya anga katika mji huo wa Syria.

Hujuma hizo za Wazayuni usiku wa Jumatatu iliyopita zilipelekea watu 17 kuuawa shahidi, akiwemo Saeed Abyar, mshauri wa kijeshi wa  Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran. Watu wengine 15 wa walijeruhiwa.

Meja Jenerali Salami amesema mashambulizi na uvamizi wa utawala wa Kizayuni nchini Syria unakanyaga sheria za kimataifa, Hati ya Umoja wa Mataifa mbali na kuwa tishio kubwa kwa amani na uthabiti wa eneo la Asia Magharibi.

Amesema, "Watenda jinai wa Kizayuni wanaoua watoto wanapaswa kufahamu kuwa, watalipa gharama ya kumwaga damu za watu wasio na hatia katika jinai hii; wanapasa kusubiri jibu (la Iran)."   

Kamanda Salami ameuhutubu utawala wa Kizayuni kwa kufanya jinai hiyo ya kutisha huko Halab na kusema: Mnapaswa kufahamu kuwa, mkitoa vitisho dhidi ya usalama wa Iran, tutakuwa na machaguo mengi. 

Kabla ya Aleppo (Halab) kukabiliwa na mradi wa uasi ulioanza kutekelezwa na maadui mwaka 2011, ulichukuliwa kuwa mji mkuu wa kiuchumi wa Syria. Mji huo ulinawiri kiuchumi kabla ya maadui kuanza kutekeleza njama za kuiangusha serikali halali ya Rais Bashar al-Assad.

3488632

Habari zinazohusiana
Kishikizo: IRAN irgc israel Salami
captcha