IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Zahra Ansari wa Iran yuko Dubai kushiriki Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani kwa Wanawake

22:12 - September 09, 2024
Habari ID: 3479407
IQNA - Zahra Ansari anaiwakilisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Toleo la 8 la Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Sheikha Fatima Bint Mubarak kwa wanawake.

Mashindano hayo yalianza huko Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu, siku ya Jumamosi, kwa kushirikisha wanawake wahifadhi Qur'ani kutoka nchi 60.

Ansari ameandamana na babake wakati wa safari yake ya kwenda Dubai.

Alizaliwa mwaka wa 2003 na  mwanafunzi wa ualimu katika Chuo Kikuu cha Farhangian.

Ansari alishika nafasi ya pili katika kategoria ya kuhifadhi Qur'ani nzima katika toleo la 46 la Mashindano ya Kitaifa ya Qur'ani ya Iran.

Mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya Sheikha Fatima Bint Mubarak kwa wanawake yataendeshwa hadi Septemba 13 katika Jumuiya ya Utamaduni na Kisayansi huko Dubai.

Tuzo la Kimataifa la Qur'ani Tukufu la Dubai (DIHQA) kila mwaka huandaa tukio la kimataifa la Qur'ani kwa wanawake kutoka nchi mbalimbali.

Zamu ya Ansari ya kuonyesha umahiri wake wa kuhifadhi Quran katika mashindano ya kimataifa itakuja Jumatano.

4235585

Habari zinazohusiana
captcha