IQNA

Muqawama

Mufti wa Oman apongeza kuchaguliwa Sheikh Qassem kama kiongozi wa Hizbullah

9:18 - November 05, 2024
Habari ID: 3479702
IQNA - Mufti Mkuu wa Oman amempongeza Sheikh Naim Qassem kwa kuteuliwa kuwa katibu mkuu mpya wa harakati ya muqawama ya Hizbullah ya Lebanon.

Katika ujumbe aliouandika kwenye akaunti yake ya X, Sheikh Ahmed bin Hamad Al Khalili alipongeza uteuzi huo.
Alisema anafurahi kwamba pengo lililopatikana baada ya kuuawa  shahidi Sayed Hassan Nasrallah imejazwa baada ya kuchaguliwa kwa Sheikh Qassem.
Sheikh Al Khalili amesema mkuu huyo mpya wa Hizbullah ataendeleza njia ya shahidi Nasrallah katika kukabiliana na hujuma za kikatili za utawala wa Kizayuni dhidi ya Lebanon na mataifa mengine ya kieneo.
Vile vile alitumai kuwa Sheikh Qassem atatekeleza jukumu hilo kwa uthabiti, ushujaa na subira hadi ushindi wa mwisho na ukombozi wa ardhi za Waislamu kutoka kwa utawala ghasibu wa Israel.
Wiki iliyopita, Sheikh Qassem, ambaye alihudumu kama naibu mkuu wa Hizbullah tangu 1991, alichukua nafasi ya Shahidi  Nasrallah, ambaye aliuawa shahidi katika shambulio la kigaidi la utawala haramu wa Israel kwenye kitongoji cha Beirut mnamo Septemba 27.
Sheikh Qassem alikuwa miongoni mwa watu waliochangia kuanzishwa kwa Hizbullah na harakati ya Amal.
 
4246173

captcha