IQNA

Sheikh Qassem: Hizbullah haitaweka chini silaha, haitaruhusu Israel kushambulia Lebanon itakavvyo

15:42 - August 26, 2025
Habari ID: 3481139
IQNA – Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sheikh Naim Qassem, amesisitiza tena msimamo wa harakati hiyo kukataa wito wa kusalimisha silaha zake.

Akizungumza katika hotuba iliyosambazwa kupitia runinga kutoka mji mkuu wa Lebanon, Beirut, jioni ya Jumatatu, Sheikh Qassem aliitaka serikali ya Lebanon kurejesha uhuru wa taifa hilo la Kiarabu, akisisitiza kuwa kundi lake halitaweka silaha zake chini na halitaruhusu adui wa Israeli kushambulia na kuteka Lebanon itakavyo.

Amesema kwamba matatizo ya ndani ya Lebanon yanaweza kutatuliwa tu pale ambapo uhuru kamili utarejeshwa.

Alisisitiza kwamba serikali inapaswa kuweka kipaumbele uhuru na ujenzi upya kuliko kufuata maelekezo ya Marekani na Israeli.

Sheikh Qassem alielezea kuingilia kati kupita kiasi kwa Washington katika masuala ya ndani ya Lebanon, akisema kuwa ndiyo chama kinachoshinikiza kwa nguvu kutaka Hizbullah isalie bila silaha, licha ya ukweli kwamba harakati ya upinzani inailinda ardhi, usalama, na uhuru wa Lebanon kwa silaha zake.

Kiongozi wa Hezbollah alitoa mwito kwa maafisa wa Lebanon kusitisha kufanya makosa, akiwakumbusha kwamba jukumu la kundi lake la upinzani sasa ni muhimu zaidi kuliko wakati wowote.

Alisema kwamba Hizbullah iliweza kuchukua nafasi muhimu katika ukombozi wa maeneo ya mashariki ya Lebanon kutoka kwa udhibiti wa Daesh na makundi mengine ya kigaidi na ya kitakfiri.

Sheikh Qassem alisema kuwa Hizbullah bado ni nguzo muhimu katika ulinzi wa usalama na heshima ya taifa la Lebanon, akisisitiza kuwa jukumu lake limekuwa muhimu zaidi, hasa katika muktadha wa ongezeko la mashambulizi ya kigeni na kuingilia kati.

Alionya kuwa utawala wa Israeli unaweza kuteka sehemu za ardhi ya Lebanon, kuua raia, na kuharibu majengo wakati wowote, lakini Hizbullah itakabiliana vikali na mipango hiyo.

Hezbollah Secretary General Sheikh Naim Qassem

Sheikh Qassem alisema kuwa kuipokonya Hizbullah silaha zake wakati adui wa Kizayuni anajaribu kuivamia na kuiangamiza Lebanon ni kinyume na mkataba wa kitaifa.

Alikataa vikali wazo la kuilazimisha Hizbullah kuweka silaha zake chini hatua hatua, akisema mawazo kama hayo ni mapema mpaka upande mwingine utimize wajibu wake na kuchukua hatua za kusitisha uhasama

Kiongozi wa Hizbullah amesisitiza kuwa Israel lazima kwanza iondoke kutoka maeneo ya Lebanon, vyeue wafungwa, na kusitisha mashambulizi.

Sheikh Qassem alisisitiza kwamba silaha za kundi la upinzani si tu ishara ya heshima ya kitaifa, bali pia zinatoa kinga dhidi ya mashambulizi ya Kizayuni.

“Mkifanya kweli kutaka uhuru, basi simamisheni mashambulizi. Hatutaacha silaha zinazotuheshimu, wala silaha zinazotulinda dhidi ya adui wetu,” alisema Sheikh Qassem.

Hezbollah, aliongeza, hufanya kazi kwa ushirikiano na Jeshi la Lebanon, ambalo alielezea kama nguvu kuu inayohusika na ulinzi wa Lebanon.

Harakati ya upinzani, alisema Sheikh Qassem, hutenda kama mfumo wa msaada unaokamilisha jeshi, hasa wakati wa mizozo.

“Ikiwa serikali hii itaendelea kama ilivyo sasa, haiwezi kuaminika kulinda uhuru wa Lebanon,” aliongeza.

Sheikh Qassem alihitimisha kwa kutoa mwito kwa wananchi wa Lebanon, viongozi wa kisiasa, na wanaharakati wa mitandao ya kijamii kuchukua jukumu muhimu zaidi katika kurejesha uhuru wa kitaifa.

3494385

Habari zinazohusiana
captcha