IQNA

Chuo Kikuu cha Ahl-ul-Bayt Tehran kimeandaa futari ya Kimataifa

15:45 - March 03, 2025
Habari ID: 3480296
IQNA – Tamasha la pili la Futari ya Kimataifa litafanyika katika Chuo Kikuu cha Ahl-ul-Bayt (AS) jijini Tehran wiki ijayo.

Wanafunzi wa kimataifa wa chuo hicho watawasilisha vyakula vya iftar kutoka nchi zao katika tamasha hili.

Wanafunzi hao wanawakilisha zaidi nchi 50 kutoka maeneo yote ya dunia

Naibu Waziri wa Sayansi, Utafiti, na Teknolojia wa Iran Saeed Habiba pamoja na baadhi ya watu mashuhuri na mabalozi kutoka nchi za Kiislamu nchini Iran watakuwepo katika tamasha hilo, ambalo limepangwa kufanyika Jumapili, Machi 9, 2025.

Iftar ni mlo wa jioni unaoashiria kumalizika saumu yaWaislamu katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani wakati wa adhana  ya sala ya Maghribi.

Ramadhani ni mwezi wa tisa katika kalenda ya Kiislamu. Ni kipindi cha sala, kufunga, kutoa sadaka na kujihesabu kwa Waislamu kote ulimwenguni.

Wakati wa Ramadhani, Waislamu hufunga (kujizuia na chakula na vinywaji) kuanzia alfajiri hadi machweo wanapovunja mfungo wao.

/3492114

Habari zinazohusiana
captcha