Kwa mujibu wa tovuti ya An-Naba, mashindano haya yatakuwa chini ya usimamizi wa Sheikh Ahmad Al-Tayyib, Imamu Mkuu wa Al-Azhar, kwa kushirikiana na Benki ya Kiislamu ya Faisal.
Sheikh Abdul Munim Fuad, ambaye ni Msimamizi Mkuu wa Shughuli za Kielimu katika taasisi ya Al-Azhar, alisema kuwa mashindano haya yamepangwa kwa makundi tofauti ya umri, na wale wanaopenda kushiriki wanahimizwa kutembelea tovuti rasmi ya Al-Azhar kwa ajili ya kujisajili.
Ameeleza kuwa mashindano haya ni fursa adhimu kwa washiriki kupima uwezo wao wa kuhifadhi Qur’ani Tukufu na kuimarisha umahiri wao katika masomo ya Qur’ani.
Kwa upande mwingine, Sheikh Hani Awdah, msimamizi wa Msikiti Mkuu wa Al-Azhar, alisema kuwa teknolojia ya sauti na video itatumika katika mchakato wa tathmini ya washiriki ili kuhakikisha uwazi na haki kwa wote.
Ameongeza kuwa zaidi ya pauni milioni moja na nusu za Kimisri zimetengwa kama zawadi kwa washindi bora kutoka katika makundi mbalimbali ya umri.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mashindano yatahusisha makundi yafuatayo:
Kuhifadhi Qur’ani yote kwa Tajweed kwa kundi la umri wa miaka 22 hadi 28
Kuhifadhi Qur’ani yote kwa Tajweed kwa walio chini ya miaka 15
Kuhifadhi thuluthi mbili (2/3) ya Qur’ani kwa walio chini ya miaka 12
Kuhifadhi thuluthi moja (1/3) ya Qur’ani kwa walio chini ya miaka 10
Usajili utaendelea kwa muda wa siku kumi kupitia tovuti rasmi ya Al-Azhar, na vituo vya mitihani vimewekwa katika mikoa mbalimbali ya Misri ili kurahisisha ushiriki wa mahafidhina kutoka maeneo yote ya nchi.
3494139/