IQNA

Mashindano ya 7 ya Kitaifa la Kuhifadhi Qur’ani nchini Ghana

15:46 - April 28, 2026
Habari ID: 3482174
IQNA – Mashindano ya Saba Ya Kitaifa la Kuhifadhi Qur’ani Tukufu nchini Ghana lilifanyika mwishoni mwa juma lililopita katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.

Tawi la Ghana la Taasis ya Mohammed VI kwa Wanazuoni wa Afrika lilifanikiwa kuandaa Shindano lake la 7 la Kila Mwaka la Kitaifa la Kuhifadhi Qur’ani, likithibitisha dhamira yake ya kuendeleza elimu ya Kiislamu, malezi ya maadili mema, na kuimarisha umoja miongoni mwa jamii za Kiislamu.

Hatua ya awali ya kitaifa iliwaleta pamoja wahifadhi mahiri wa Qur’ani kutoka sehemu mbalimbali za nchi, pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanaoheshimika na viongozi wa kimila.

Hafla hiyo ilifanyika siku ya Jumamosi, tarehe 25 Aprili 2026, katika ukumbi wa Islamic Council for Development & Humanitarian Services (ICODEHS) uliopo Kotobabi, Accra.

Mashindano hayo ni sehemu ya juhudi pana za bara la Afrika zinazolenga kuimarisha uelewa wa dini na ushiriki wa kielimu miongoni mwa Waislamu barani humo.

Waandaaji walieleza kuwa lengo la mashindano ni kuhamasisha kuhifadhi na kusoma Qur’ani Tukufu kwa usahihi, sambamba na kuwahimiza vijana wa Kiislamu kuyafanya mafundisho ya Qur’ani kuwa mwongozo wa ukuaji wao binafsi na maendeleo ya jamii.

Mpango huo pia unakusudia kukuza maadili ya amani, nidhamu na ubora wa kiroho, pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za Kiislamu katika bara zima.

Katika mashindano ya mwaka huu, washiriki walionesha kiwango cha juu sana cha umahiri, wakidhihirisha ustadi mkubwa katika mitindo ya qira’a na usahihi wa kuhifadhi Qur’ani. Watazamaji walibainisha kuwa ubora wa washiriki ulionyesha maandalizi makini pamoja na kujitolea kwa dhati katika ibada.

Washindi katika Makundi Matatu

Mashindano yalikuwa na makundi matatu makuu, na washindi wake walikuwa kama ifuatavyo:

• Makundi ya Juzuu Tano za Qur’ani

Nafasi ya Kwanza: Sufyan Abdul‑Aziz

Nafasi ya Pili: Rahma Ibrahim

Nafasi ya Tatu: Sudais Uthmam

• Hifdh ya Qur’ani Nzima (Qira’a ya Warsh)

Nafasi ya Kwanza: Abdul‑Muhaimin Ramadan Sharafudeen

Nafasi ya Pili: Ibrahim Abdul‑Salam

Nafasi ya Tatu: Ahmad Mohammed

• Kundi la Qira’a ya Hafs na Riwaya Nyingine

Nafasi ya Kwanza: Zainab Abdul‑Rahman

Nafasi ya Pili: Hafiz Abdul‑Rahman

Nafasi ya Tatu: Abdul‑Hanan Mohammed

Washiriki wote walipokea zawadi ya nakala za Qur’ani Tukufu, vitabu vya Kiislamu na zawadi za fedha taslimu, huku washindi wa juu wakipewa tuzo maalumu.

Washindi wa kila kundi wataiwakilisha Ghana katika Mashindano ya Qur’ani ya Afrika nzima yatayoandaliwa chini ya usimamizi wa Taasis ya Mohammed VI kwa Wanazuoni wa Afrika nchini Morocco. Mahali na tarehe ya mashindano hayo ya bara zima vitatangazwa baadaye.

Mashindano hayo ya kila mwaka yanaendelea kuwa jukwaa muhimu la kukuza ubora wa kielimu na kiroho, pamoja na kuchangia maelewano ya kijamii na kuishi kwa amani nchini Ghana na katika bara la Afrika kwa ujumla.

3497257

captcha