waislamu - Ukurasa 65

IQNA

TEHRAN (IQNA) –Wataalamu 22 wa Qur'ani Tukufu kutoka nchi 13 za kigeni wameteuliwa kuwa majaji katika Mashindano ya 36 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3471859    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/03

TEHRAN (IQNA) – Katika kipindi cha siku kadhaa sasa kumeibuka uhasama mkubwa baina ya India na Pakistan na kuna hatari ya kuibuka vita kamili baina ya madola hayo mawili yenye makombora ya nyuklia.
Habari ID: 3471856    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/28

TEHRAN (IQNA). Sherehe za Mazazi ya Bibi Fatima Zahra SA hivi karibuni zimewaleta pamoja Waislamu na wapenzi wa Ahul Bayt wa Mtume SAW katika katika Markaz Mafaatihul Jinaan, Kiguza, Mkuranga, Pwani nchini Tanzania.
Habari ID: 3471854    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/26

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema wakati alipoonana na kuzungumza na Rais Bashar al Assad wa Syria hapa mjini Tehran Jumatatu kwamba, Iran inalihesabu suala la kuiunga mkono Syria kuwa ni sawa na kuunga mkono muqawama (mapambano ya Kiislamu) na inaona fakhari kwa jambo hilo.
Habari ID: 3471853    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/26

TEHRAN (IQNA)- Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamemkamata mkuu wa Idara ya Wakfu inayosimamia maeneo matakatifu ya Kiislamu katika mji wa Quds (Jerusalem) .
Habari ID: 3471852    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/25

TEHRAN (IQNA)-Kufuatia ongezeko la wageni Waislamu nchini Japan, vyumba vya Sala vya Waislamu vinawekwa katika maeneo mengi ya kibiasahra kote katika nchi hiyo.
Habari ID: 3471851    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/24

TEHRAN (IQNA)- Magaidi wakufurishaji wa Boko Haram mapema leo wameshambulia mji katika eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuwalazimu wakazi kutoroka masaa machache tu kabla ya kuanza upigaji kura katika uchaguzi mkuu.
Habari ID: 3471850    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/23

TEHRAN (IQNA) – Katika tukio ambalo limetajwa kuwa la kihistoria na la aina yake nchini Kenya, msikiti umejengwa katika sehemu ilimokuwa imejengwa kanisa baada ya askofu wa kanisa hilo kusilimu na wafuasi wake.
Habari ID: 3471849    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/22

TEHRAN (IQNA) –Serikali ya China inaendeleza ukandamizaji wake wa jamii ya Waislamu nchini humo na sasa inatumia kamera maalumu kwa lengo la kuwachunguza na kuwadhibiti Waislamu.
Habari ID: 3471848    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/21

TEHRAN (IQNA)- Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel Jumanne waliuhujumu Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) na kuwajeruhi Wapalestina waliokuwa wakifanya ibada katika eneo hilo la tatu kwa utakatifu katika Uislamu.
Habari ID: 3471847    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/20

TEHRAN (IQNA)- Serikali ya Sudan imeanza mradi wa kitaifa wa kukarabati nakala za kale za Qur'ani Tukufu.
Habari ID: 3471844    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/17

TEHRAN (IQNA)- Mahakama nchini Austria imebatilisha uamuzi wa serikali kufunga misikiti sita ya jamii ya Waarabu nchini humo.
Habari ID: 3471842    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/15

TEHRAN (IQNA) – Washindi wa Mashindano ya Qur'ani ya watoto walemavu yamefanyika nchini Saudi Arabia.
Habari ID: 3471839    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/13

Baada ya kufanya utafiti
TEHRAN (IQNA)- Mwanasiasa wa mrengo wa kulia na mbunge wa zamani UholanzI, Joram van Klaveren aliyekuwa na chuki kubwa dhidi ya Uislamu ameibua gumzo nchini humo baada ya kutangaza kubadilisha msimamo wake na kusilimu.
Habari ID: 3471832    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/06

TEHRAN (IQNA)-Fainali za Mashindano ya 36 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu zimepangwa kuanza mjini Tehran kuanzia Aprili 10.
Habari ID: 3471831    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/05

TEHRAN (IQNA)- Siku ya Kimataifa ya Hijabu imeadhimishwa Ijumaa katika mji wa Lamu nchini Kenya huku washiriki wakitoa wito wa kuondolewa marufuku ya Hijabu shuleni nchini humo.
Habari ID: 3471828    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/03

TEHRAN (IQNA)- Idara ya Mfawidhi wa Haram Takatifu ya Imam Hussein AS iliyoko nchini Iraq imezindua Taasisi ya Qur'ani nchini Burkina Faso.
Habari ID: 3471827    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/02

Waziri Mkuu Mahathir Mohamad
TEHRAN (IQNA)-Waziri Mkuu wa Malaysia Mahathir Mohammad amesisitiza Jumatatu kuwa nchi yake inashikilia msimamo wake wa kuwazuia raia wa utawala haramu wa Israel kuingia nchini humo huku akiitaja Israel kuwa utawala wa kihalifu.
Habari ID: 3471824    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/01/29

TEHRAN (IQNA)- Hatimaye utawala wa Marekani umelazimika kumuachulia huru bila kumfugulia mashtaka mtangazaji wa Press TV, Bi. Marzieh Hashemi baada ya kumshikilia kizuizini kinyume cha sheria kwa muda wa siku 11.
Habari ID: 3471818    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/01/24

TEHRAN (IQNA)-Msikiti wa Jamia katika mji mkuu wa Russia, Moscow, umeanzisha mpango maalumu wa kusoma (qiraa) Qur'ani Tukufu kwa muda wa masaa 24 kila siku.
Habari ID: 3471815    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/01/22