waislamu - Ukurasa 64

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Fainali za Mashindano ya 36 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimeanza rasmi Jumatano alasiri katika halfa iliyofanyika mjini Tehran.
Habari ID: 3471909   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/04/10

TEHRAN (IQNA) - Picha za satalaiti zinaonyesha kuwa serikali ya China inabomoa misikiti muhimu ya eneo lenye Waislamu wengi la Xinjiang.
Habari ID: 3471908   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/04/10

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Marekani inahasimiana na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kwa sababu jeshi hilo limekuwa mstari wa mbele katika kuilinda Iran na Mapinduzi ya Kiislamu na kuongeza kuwa: "Kwa miaka 40 sasa, Marekani na maadui wengine wajinga wamekuwa wakifanya kila wawezalo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran lakini wameshindwa."
Habari ID: 3471906   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/04/09

TEHRAN (IQNA) – Washiriki wa Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wameanza kuwasili nchini.
Habari ID: 3471904   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/04/08

TEHRAN (IQNA)- Idara ya Polisi nchini Ireland imeamua kuwaruhusi maafisa wa polisi kike ambao ni Waislamu kuvaa vazi la staha la Hijabu.
Habari ID: 3471900   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/04/06

TEHRAN (IQNA)- Mfalme Salman Bin Abdulaziz wa Saudi Arabia ameitembelea Bahrain katika safari fupi na kufanya mazungumzo na mfalme wa nchi hiyo Hamad bin Isa Aal Khalifa.
Habari ID: 3471898   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/04/04

TEHRAN (IQNA)- Shule ya Waislamu mjini New Castle Uingereza imehujumiwa na watu wenye chuki dhidi ya Uislamu ambao walivunjia haeshima nakala za Qur'ani Tukufu katika shule hiyo.
Habari ID: 3471891   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/28

Kiongozi wa Hizbullah Hassan Nasrallah
TEHRAN (IQNA)-Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuitambua rasmi miinuko ya Golan kuwa ni miliki ya utawala bandia wa Israel ni kuzitusi na kuzivunjia heshima nchi za Ulimwengu wa Kiislamu na Kiarabu.
Habari ID: 3471890   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/27

TEHRAN (IQNA)- Waziri Mkuu wa New Zealand Jacind Ardern ameagiza kufanyike uchunguzi huru kuhusu hujuma za kigaidi dhidi ya misikiti miwili katika mji wa Christchurch nchini humo.
Habari ID: 3471888   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/26

TEHRAN (IQNA)-Rais Donald Trump wa Marekani amelaani vikali na kutengwa kimataifa kudai kuwa kuwa utawala haramu wa Israel unamiliki miinuko ya Golan ya Syria.
Habari ID: 3471887   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/24

TEHRAN (IQNA)- Kikao cha dharura cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kimefanyika Ijumaa mjini Istanbul, Uturuki kwa lengo la kujadili hatua za kuchukuliwa baada ya shambulio la kigaidi la hivi karibuni dhidi ya Waislamu waliokuwa katika Sala ya Ijumaa kwenye misikiti miwili nchini New Zealand.
Habari ID: 3471886   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/23

TEHRAN (IQNA)-Serikali ya Uingereza imetakiwa kuwapa Waislamu ulinzi kufuatia hujuma za Ijumaa iliyopita dhidi ya misikiti miwili nchini New Zealand.
Habari ID: 3471882   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/20

TEHRAN (IQNA) – Waziri Mkuu wa Malaysia Mahathir Mohammad amesema baadhi ya Waislamu hawana ufahamu sahihi wa Qur'ani na hivyo wanajihusisha na vitendo vilivyo kinyume cha mafundisho ya Uislamu.
Habari ID: 3471880   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/18

TEHRAN (IQNA) – Pale waumini walipokuwa wakimiminiwa risasi na gaidi wakati wa Sala ya Ijumaa msikitini, dereva wa texi, Abdul Kadir Ababora, alijificha chini ya rafu ambayo hutumika kuweka nakala za Qur'ani Tukufu huku akiomba Duaa kuwa apate fursa ya kubakia na mke na watoto wake.
Habari ID: 3471879   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/17

TEHRAN (IQNA)-Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali hujuma za kigaidi zilizolenga misikiti miwili jana mjini Christchurch New Zealand na kupelekea Waislamu wasiopungua 49 kuuawa shahidi wakiwa katika Sala ya Ijumaa.
Habari ID: 3471878   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/16

TEHRAN (IQNA)-Nchi 82 zinatazamiwa kuwa na wawakilishi katika Mashidani ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu nchini Iran mwaka huu.
Habari ID: 3471875   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/14

TEHRAN (IQNA)- Watoto wa shule moja ya chekechea ya Wakristo mjini Dusseldorf nchini Ujerumani wataanza kufunzwa Uislamu.
Habari ID: 3471872   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/12

TEHRAN (IQNA)- Waislamu nchini Marekani wanabaguliwa zaidi ya wafuasi wa dini zingine zote nchini humo.
Habari ID: 3471870   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/10

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuhusu kuwepo uthabiti na amani nchini Myanmar. Aidha amesisitiza kuwa wakimbizi Waislamu wa jamii ya Rohingya warejeshwe haraka na kwa usalama katika makazi yao nchini Myanmar.
Habari ID: 3471869   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/09

TEHRAN (IQNA)-Wananchi wa matabaka mbali mbali huko Algeria wameendeleza maandamani Ijumaa wakimtaka Rais Abdelaziz Bouteflika aondoke madarakani na asiwanie tena urais mwezi ujao wa Aprili.
Habari ID: 3471867   Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/08