TEHRAN (IQNA)- Mjumbe wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina nchini Iran Nasser Abu Shariff ametembelea ofisi za Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa (IQNA) hapa mjini Tehran.
Habari ID: 3473579 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/21
TEHRAN (IQNA)- Gazeti moja la Kiebrania limeripoti kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umetoa sharti kwa Uturuki la kuifunga ofisi ya HAMAS mjini Istanbul ili kuanzisha tena uhusiano kamili na nchi hiyo.
Habari ID: 3473570 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/19
TEHRAN (IQNA) - Harakati za kupigania ukombozi wa Palestina za Fat'h na Hamas zimeunga mkono tangazo la Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuhusu kufanyika uchaguzi wa bunge la rais baadaye mwaka huu.
Habari ID: 3473561 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/16
TEHRAN (IQNA)- Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wamesema utawala wa Israel, kama utawala vamizi unaokali ardhi za Palestina kwa mabavu, unapaswa kuwapa Wa palestina chanjo ya corona.
Habari ID: 3473559 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/15
TEHRAN (IQNA) - Mwakilishi wa harakati ya Jihadul Islami ya kupigania ukombozi wa Palestina nchini amepongeza nafasi ya Luteni Jenerali Shahidi Qassem Soleimani katika kuwaunganisha Wa palestina .
Habari ID: 3473552 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/13
TEHRAN (IQNA) - Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetahadharisha kuhusu mpango wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kubomoa sehemu za Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem).
Habari ID: 3473547 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/11
TEHRAN (IQNA)- Utawala wa Kizayuni wa Israel umeongeza maradufu kasi ya kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi ulizowapora Wa palestina hatua ambayo itaibua msuguano na serikali mpya ijayo ya Marekani.
Habari ID: 3473545 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/11
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi mwandamizi Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amewaomba baadhi ya viongozi wa nchi ikiwemo Iran kuunga mkono juhudi zilizofanyika kwa ajili ya kuimaisha umoja na mshikamano wa kitaifa wa Palestina.
Habari ID: 3473544 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/10
TEHRAN (IQNA) - Makumi ya wabunge wa Algeria wameandaa muswada wa sheria inayolenga kuufanya kuwa ni uhalifu uanzishwaji wa uhusiano wowote wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3473536 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/08
TEHRAN (IQNA)- Wa palestina katika Ukanda wa Ghaza wameandaa khitma kwa mnasaba wa kuwadia mwaka moja tokea auawe shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani.
Habari ID: 3473528 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/05
TEHRAN (IQNA) - Jumuiya ya Kimataifa ya Maulamaa wa Kiislamu (IUMS) imetoa fatua ya kuususia kikamilifu utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na kutangaza kwamba, haijuzu kuuuzia wala kununua chochote kinachozalishwa na utawala huo mpaka utakapokomesha ukaliaji wake ardhi kwa mabavu.
Habari ID: 3473524 Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/04
TEHRAN (IQNA)- Balozi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa ametuma barua tofauti kwa viongozi wa umoja huo akitaka jamii ya kimataifa kukabiliana ipasavyo na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel na kuuadhibu utawala huo kwa hatua yake ya kuendeleza ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina.
Habari ID: 3473508 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/30
TEHRAN (IQNA) – Wa palestina katika Ukanda wa Ghaza wamemuenzi Shahidi Luteni Jeneali Qassem Soleimani mwaka mmoja baada ya kuuawa kwake katika hujuma ya jeshi la kigaidi la Marekani katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad.
Habari ID: 3473505 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/29
Jumuiya ya Maulama wa Kiislamu Duniani
TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Kimataifa ya Maulamaa Waislamu (IAMS) amesema kuwa, viongozi wanaotaka mapatano wameanzisha uhusiano wa kawaida na Israel kwa sababu ya woga, tamaa na kwa ajili ya kulinda maslahi yao pamoja na tawala zao, hatua ambayo ni haramu na batili.
Habari ID: 3473502 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/28
Harakati ya Kiislamu ya Amal ya Jordan
TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Kiislamu ya Amal ya Jordan imetoa taarifa na kusema hatua ya Morocco kuafiki kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel ni kashfa kubwa na pia ni uhaini wa kihistoria.
Habari ID: 3473491 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/25
TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kitendo cha baadhi ya nchi za Kiarabu cha kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel ni kuwasaliti wananchi wa Palestina na umma wa Kiislamu kwa ujumla.
Habari ID: 3473488 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/24
TEHRAN (IQNA) – Indoneisa imekanusha ripoti kuwa iko tayari kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia na utawala bandia wa Israel.
Habari ID: 3473487 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/24
TEHRAN (IQNA) - Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Tunisia imeashiria juhudi za baadhi ya mataifa ya kieneo za kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel na kusisitiza kwamba, serikali ya Tunis haina mpango wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala huo ghasibu.
Habari ID: 3473484 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/23
TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Kamati Kuu ya Mapinduzi ya Wananchi wa Yemen ameashiria kuendelea kuchimbwa mashimo na njia za chini kwa chini kuelekea katika msikiti mtakatifu wa al-Aqswa ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu na kueleza kwamba, Waislamu wanapaswa kutumia nyenzo na suhula zote kukabiliana na njama hizo.
Habari ID: 3473483 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/23
TEHRAN (IQNA) -Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, sera za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) za kuunga utawala wa Kizayuni wa Israel ni kwa madhara ya haki za Wa palestina .
Habari ID: 3473477 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/21