iqna

IQNA

TEHRAN (IQNA) - Mfalme Abdullah wa Pili wa Jordan ameutahadharisha utawala wa Israel kuwa utaraji mapigano makubwa iwapo utasonga mbele na mpango wake wa kuteka zaidi ardhi za Palestina katika Ukingo wa Magharibi na Bonde la Jordan.
Habari ID: 3472774    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/17

TEHRAN (IQNA) - Wizara ya Mambo ya Nje Iran imetoa tamko kuhusu siku ya "Nakba" yaani siku ya nakama ya kuasisiwa utawala pandikizi wa Kizayuni katika ardhi walizoporwa Wa palestina na kusisitiza kuwa, kadhia ya Palestina itaendelea kuwa suala kuu nambari moja katika ulimwengu wa Kiislamu licha ya kufanyika njama nyingi za kulisahaulisha.
Habari ID: 3472767    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/15

TEHRAN (IQNA) – Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds ya mwaka huu yanatazamiwa kufanyika katika ukumbi wa Instagram na mitandao mingine ya kijamii nchini Afrika Kusini, kutokana na janga la corona.
Habari ID: 3472758    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/12

TEHRAN (IQNA) - Balozi wa Syria katika Umoja wa Mataifa amesema Baraza la Usalama la umoja huo limefeli kuushinikiza utawala wa Kizayuni wa Israel utekeleza maazimio ya baraza hilo kuhusu Palestina na Syria.
Habari ID: 3472699    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/24

Kufuatia janga la corona
TEHRAN (IQNA) – Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imetoa wito kwa taasisi za za kisheria Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu kuchukua hatua za dharura za kuwaokoa mateka Wa palestina wanaoshikiliwa katika jela za kuogofya za utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3472675    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/17

TEHRAN (IQNA) - Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetaka Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) ichukue hatua za dharura za kuzuia hatua za utawala wa Kizayuni wa Israel za kunyakua ardhi zaidi Wa palestina katika mji wa Quds (Jerusalem) na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Habari ID: 3472661    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/13

TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema harakati hiyo imeazimia kuhakikisha kuwa mateka wa Ki palestina walioko katika vizuizi vya utawala wa Kizayuni wa Israel wanaachiwa huru katika mpango wa kubadilishana wafungwa na utawala huo ghasibu.
Habari ID: 3472652    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/10

TEHRAN (IQNA) – Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imetoa wito kwa mashirika ya kutetea haki za binadamu na asasi zingine za dunia kuushinikiza utawala wa Kizayuni wa Israel uwaachilie huru Wa palestina inaowashikilia katika magereza yake ili wasiambukizwe ugonjwa wa COVID-19 au corona ambao umeenea katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel).
Habari ID: 3472601    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/25

TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amemuandikia barua Mfalme Salman wa Saudia na kusitiza juu ya ulazima wa kuachiliwa huru haraka iwezekanavyo wafungwa wa Ki palestina wanaoshikiliwa nchini Saudi Arabia.
Habari ID: 3472596    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/23

TEHRAN (IQNA) - Utawala wa Kizayuni wa Israel umemkamata Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Wakfu wa Kiislamu katika mji wa Quds (Jerusalem) huku kukiwa na tetesi kuwa Wazayuni wanalenga kumuambukjiza kirusi cha corona.
Habari ID: 3472571    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/16

TEHRAN (IQNA) – Kiongozi wa Harakati ya Mapmbano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas), Ismail Haniya amesema Russia inapinga mpango wa 'muamala wa karne' uliowasilishwa na Mareknai kuhusu kadhia ya Palestina.
Habari ID: 3472528    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/04

Makundi ya Palestina
TEHRAN (IQNA) –Makundi ya muqawama au kupigania ukombozi wa Palestina yamesisitiza kuwa, matokeo ya awali ya uchaguzi wa bunge katika utawala wa Kizayuni wa Israel yanayoneysha kuwa hakuna mabadiliko yoyote katika sera za utawala huo.
Habari ID: 3472526    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/03

Malefu ya Wapalestina washiriki katika Sala ya Ijumaa Msikiti wa Al Aqsa
TEHRAN (IQNA) - Maelfu ya Wa palestina walishiriki katika Salatul Fajr katika Msikiti wa Al Aqsa mjini Quds (Jerusalem) Ijumaa asubuhi licha ya vizuizui vikali vilivyokuwa vimewekwa na jeshi la utawala wa Kizyauni wa Israel.
Habari ID: 3472514    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/29

TEHRAN (IQNA) - Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel jana Jumapili lilishambulia kwa mizinga eneo la Ukanda wa Ghaza na kumuua shahidi kijana wa Ki palestina , Mohammed Ali al-Naim aliyekuwa na umri wa miaka 27.
Habari ID: 3472502    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/24

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
TEHRAN (IQNA) - Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kusimama kidete katika njia ya muqawama au mapambano na njia ya demokrasia ya kuitishwa kura ya maamuzi ili Wa palestina wenyewe waamue mustakabali wao ndilo suluhisho la kadhia ya Palestina.
Habari ID: 3472483    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/18

TEHRAN (IQNA) - Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imetangaza orodha ya mashirika ambayo yanashirikiana na utawala wa Israel katika kujenga vitongoji haramu katika ardhi za Palestina huko Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Habari ID: 3472468    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/13

TEHRAN (IQNA) – Makumi ya walowezi wa Kizayuni wameuhujumu Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3472467    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/13

TEHRAN (IQNA) - Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa, mbali na mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani uliopewa jina la Muamala wa Karne kukanyaga maazimio ya umoja huo, pia ni wa kibaguzi na unakiuka mamlaka na uhuru wa kujitawala Palestina.
Habari ID: 3472464    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/12

TEHRAN (IQNA) - Ismail Haniya Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amemtumia ujumbe Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na akimpongeza yeye na taifa la Iran kufuatia maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Habari ID: 3472463    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/12

Rais wa Afrika Kusini
TEHRAN (IQNA) - Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amesema mapendekezo ya Rais Donald Trump kwenye 'muamala wa karne' kuhusu Palestina yanashabihiana na mfumo wa kipindi cha utawala wa ubaguzi wa rangi (apatheidi) uliowahi kutawala nchi yake.
Habari ID: 3472459    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/10