iqna

IQNA

TEHRAN (IQNA) - Viongozi wa Afrika wameulaani mpango uliopendekezwa na Rais Donald Trump wa Marekani ambao ni maarufu kama 'muamala wa karne' kuhusu utatuzi wa mgogoro wa Israel na Palestina na kuutaja kuwa usio na uhalali.
Habari ID: 3472455    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/09

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, mpango wa Marekani uliopachikwa jina la Muamala wa Karne utakufa hata kabla ya Trump mwenyewe kufa na kuongeza kuwa, njia ya kukabiliana na mpango huo ni kusimama kidete na kufanya jihadi kishujaa taifa na makundi ya Palestina pamoja na uungaji mkono wa ulimwengu wa Kiislamu kwa taifa hilo.
Habari ID: 3472444    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/05

TEHRAN (IQNA) - Nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) zimepinga mpango wa 'muamala wa karne' uliopendekezwa na Marekani ambao unakandamiza haki za taifa la Palestina.
Habari ID: 3472435    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/03

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amekosoa tangazo la mpango wa Marekani na Israel unaojulikana kama 'muamala wa karne' kwa ajili ya kutatua kadhia ya Palestina na kusema nchi za Kiarabu katu hazitaliacha taifa la Palestina peke yake.
Habari ID: 3472429    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/01

Wananchi wa Yemen wamefanya maandamano makubwa ya kulaani njama mpya za Marekani dhidi ya taifa madhlumu la Palestina na wamelaani vikali mpango wa Donald Trump wa "Muamala wa Karne."
Habari ID: 3472424    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/31

TEHRAN (IQNA) - Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameuhujumu Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala huo na kuwajeruhi Wa palestina kadhaa waliokuwa wamefika hapo kwa ajili ya Sala ya Ijumaa.
Habari ID: 3472423    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/31

Ismail Haniya
TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano (Muqawama) ya Kiislamu ya Palestina HAMAS, Ismail Haniyeh ametuma ujumbe kwenda kwa viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu akionya ushiriki wa aina yoyote kwa ajili ya kutekelezwa au kuukubali mpango wa Muamala wa Karne na kubainisha kuwa hilo ni kosa kubwa ambalo kamwe raia wa Palestina hawatalisamehe.
Habari ID: 3472422    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/30

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema pendekezo la Marekani lililopewa jina la 'Muamala wa Karne' katu halitazaa matunda kwa Rehema za Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3472421    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/30

Katika barua maalumu
TEHRAN (IQNA) - Spika wa Bunge la Iran (Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu) ametoa wito wa kukabiliana na mpango bandia wa Rais Donald Trump uliopewa jina la "Muamala wa Karne". Aidha ametoa wito kutatuliwa mgogoro wa Palestina kwa kutumia njia ya kura ya maoni na udiplomasia wa kibunge.
Habari ID: 3472418    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/29

TEHRAN (IQNA) – Rais wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina amezitaka nchi za Kiislamu na Kiarabu kususia uzinduzi wa mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusiana na mgogoro wa Palestina uliopewa jina la "Muamala wa Karne".
Habari ID: 3472412    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/28

TEHRAN (IQNA) - Wanajeshi katili wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi kwa kuwapiga risasi Wa palestina watatu katika uzio wa Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3472396    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/22

TEHRAN (IQNA) – Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limewaua shahidi Wa palestina 149 katika mwaka uliopita wa 2019, aghalabu wakiwa katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3472322    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/01

TEHRAN (IQNA) -Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS imeunga mkono uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai unaonyesha kuwa hulka ya uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu ya Israel na kiwango cha dhulma ilizowafanyia wananchi madhulumu wa Palestina vimezidi kudhihirika mbele ya jamii ya kimataifa.
Habari ID: 3472297    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/12/23

TEHRAN (IQNA) – Mwendesha Mashtaka Mkuu katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) amesema ataanzisha uchunguzi kamili kuhusu jinai za kivita za utawala dhalimu wa Israel dhidi ya Wa palestina .
Habari ID: 3472293    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/12/21

TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imelaani vikali hatua ya utawala haramu wa Israel kukamata wanachama wake katika eneo inalolikalia kwa mabavu la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Habari ID: 3472274    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/12/13

TEHRAN (IQNA) - Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeitaja tetesi iliyoenea katika vyombo vya habari vya Kizayuni kuhusu jitihada za utawala huo za kufikia makubaliano ya usitishaji vita ya muda mrefu na Ukanda wa Ghaza kuwa ni propaganda za uchaguzi.
Habari ID: 3472257    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/12/05

TEHRAN (IQNA) – Mufti wa Waislamu wa eneo la Volgograd Oblast nchini Russia amesisitiza ulazima wa kukombolewa mji Mtakatifu wa Quds, sehemu uliko Msikiti wa Al Aqsa na kusema kutetea Quds Tukufu na Palestina kunapaswa kuwa kadhia muhimu zaidi katika ulimwengu wa Kiislamu hivi sasa.
Habari ID: 3472234    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/11/27

TEHRAN (IQNA)- Waislamu duniani wameendelea kulaani hatua ya Marekani kubadili msimamo na kuanza kuunga rasmi hatua iliyo kinyume cha sheria ya Israel ya kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina.
Habari ID: 3472224    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/11/20

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuondolewa Israel kuna maana ya kuondolewa utawala bandia wa Kizayuni na mahala pake kuchukuliwa na serikali iliyochaguliwa na wamiliki wa asili wa Palestina ambao ni Waislamu, Wakristo na Mayahudi.
Habari ID: 3472216    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/11/15

TEHRAN (IQNA)- Makamanda wawili wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina wameuawa aktika hujuma mpya za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3472213    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/11/13