iran - Ukurasa 39

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Mwanazuoni mwandamizi wa Iraq amesisitiza kuhusu ulazima wa wanazuoni na maulamaa wa Kiislamu dunaini kuwa macho ili kuzuia njama za maadui za kuchochea mifarakano baina ya Waislamu.
Habari ID: 3474452   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/21

TEHRAN (IQNA)- Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas), amesema muqawama au mapambano ndio njia bora zaidi ya kukomboa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3474447   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/20

TEHRAN (IQNA)- Rais wa Iran amesema wazo la kuzikurubisha pamoja madhehebu za Kiislamu lililobuniwa na Imam Khomeini (MA), Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ni hatua ya kistratajia katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 3474444   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/19

TEHRAN (IQNA)- Misikiti 225 kote katika mji mkuu wa Jamuri ya Kiislamu ya Iran, Tehran, imejunga na kampeni maalumu ya kuwapa chanjo waumini katik kipindi cha siku 20.
Habari ID: 3474436   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/18

TEHRAN (IQNA)- Hujjatul Islam Hamid Shahriari, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu amezungumza na waandishi habari kuhusu Kongamano la 35 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu.
Habari ID: 3474432   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/17

TEHRAN (IQNA)- Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali kitendo cha magaidi wakufurishaji kuushambulia msikiti wa Bibi Fatima wakati wa Sala ya Ijumaa mjini Kandahar nchini Afghanistan.
Habari ID: 3474428   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/16

TEHRAN (IQNA)- Mkurugenzi wa Taasisi ya Mustafa (saw) amesema kuwa wanasayansi watano Waislamu wametunukiwa tuzo ya taasisi hiyo ya mwanasayansi bora katika Ulimwengu wa Kiislamu mwaka huu wa 2021.
Habari ID: 3474418   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/13

Spika wa Bunge la Iran
TEHRAN (IQNA)- Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesisitiza kuwa vita vya vyombo vya habari vya maadui vimevizidi nguvu na kasi vita vya kiuchumi na kwamba hata maadui wa mapinduzi wananufaika na vita hivyo vya vyombo vya habari katika vita vyao vya kiuchumi dhidi ya mataifa mengine.
Habari ID: 3474416   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/12

Rais Ebrahim Raisi
TEHRAN (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema nchi hii imeweza kupata mafanikio makubwa katika sekta za ulinzi na nyuklia pamoja na kuwepo vikwazo shadidi vya maadui na hivyo vikwazo kama hivyo haviwezi kuwa kizingiti katika ustawi wa Iran.
Habari ID: 3474411   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/11

TEHRAN (IQNA)- Huku Iran ikiadhimisha wiki ya malenga mashuhuri wa Kifarsi Hafidh (Hafez au Hafiz), maonesho ya vitabu chini ya anuani ya ‘Hafez na Qur’ani’ yammefanyika katika kaburi lake ambalo ni maarufu kama Hafezieh mjini Shiraz kusini mwa Iran.
Habari ID: 3474405   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/10

TEHRAN (IQNA)- Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma ujumbe kufuatia kuuawa shahidi na kujeruhiwa idadi kubwa ya watu wasio na hatia nchini Afghanistan.
Habari ID: 3474400   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/09

TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon kuhusu matukio ya karibuni kabisa ya kisiasa ya nchi hiyo na eneo.
Habari ID: 3474395   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/08

TEHRAN (IQNA)- Kumetolewa pendekezo la kujengwa barabara kutoka mji mtakatifu wa Mashhad nchini Iran hadi mji mtakatifu wa Makka nchini Saudi Arabia.
Habari ID: 3474391   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/06

TEHRAN (IQNA)- Afisa wa ngazi ya juu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kundi hilo la muqawama lina haki ya kutumia njia zote halali kulilinda taifa la Lebanon, na kuvunja vikwazo na mzingiro wa Marekani dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
Habari ID: 3474387   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/06

TEHRAN (IQNA)- Mazungumzo baina ya Jamhuri ya Kiislamu na Ufalme wa Saudi Arabia yanaendelea vizuri kwa lengo la kutatua matatizo yaliyopo baina ya pande mbili.
Habari ID: 3474386   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/05

TEHRAN (IQNA)- Utawala wa Taliban nchini Afghanistan umetangaza habari ya kuuvunja mtandao wa genge la kigaidi la Daesh (ISIS) katika eneo la kaskazini mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Kabul.
Habari ID: 3474383   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/05

TEHRAN (IQNA) Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kikao cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi ameutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za haraka za kuhitimisha jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya Palestina.
Habari ID: 3474376   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/03

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema uingiliaji na uwepo wa askari vamizi wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) ni chanzo cha mfarakano na uharibifu katika kanda hii.
Habari ID: 3474375   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/03

TEHRAN (IQNA)- Harakati kadhaa za kupigania ukombozi wa Palestina zimelaani vikali hatua ya ufalme wa Bahrain kumpokea waziri wa mambo ya nje wa utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3474372   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/02

TEHRAN (IQNA)- Kamanda wa vikosi vya nchi kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa tangu uje utawala wa Kizayuni karibu na mipaka ya nchi, Iran imezidi kuguswa na suala la usalama wa mpaka wake wa kaskazini magharibi na kwa sababu hiyo harakati za utawala huo haramu zinafuatiliwa kikamilifu.
Habari ID: 3474367   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/01