iqna

IQNA

TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyed Ali Khamenei ametuma salamu za rambi rambi kufuatia kuaga dunia Ayatullah Muhammad Yazdi ambaye alikuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Wasomi na Wahadhiri wa Chuo cha Kidini cha Qum
Habari ID: 3473441    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/10

TEHRAN (IQNA)- Katika muendelezeo wa vikwazo vya kidhalimu vya Marekani dhidi ya Iran, Wizara ya Fedha ya nchi hiyo imetangaza vikwazo dhidi ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al Mustafa SAW na balozi wa Iran nchini Yemen Hassan Irloo.
Habari ID: 3473440    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/09

TEHRAN (IQNA) - Mwanazuoni mtajika wa Kiislamu nchini Iran, Ayatullah Muhammad Yazdi, ameaga dunia leo na kurejea kwa Mola wake.
Habari ID: 3473438    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/09

Rais wa ya Iran katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria
TEHRAN (IQNA) - Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesemam kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itaendeleza maamuzi na irada ambayo imekuwa ikichukua katika kuiunga mkono serikali na taifa la Syria kama nchi muitifakii wake wa kistratejia na itakuwa bega kwa bega na Syria hadi kupatikana ushindi wa mwisho.
Habari ID: 3473435    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/08

TEHRAN (IQNA) - Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma ujumbe kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kushikamana na Wananchi wa Palestina na kuitolea mwito jamii ya kimataifa kukabiliana na hatua za utawala wa Kizayuni wa Israel unaouwa watoto.
Habari ID: 3473415    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/02

TEHRAN (IQNA) - Wabunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) wamelitaka Shirika la Atomiki la Iran kuzalisha urani iliyorutubishwa kwa zaidi ya asilimia 20 kwa ajili ya matumizi ya amani.
Habari ID: 3473412    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/01

TEHRAN (IQNA)- Nchi na viongozi mbalimbali duninani wameendelea kulaani mauaji ya mwanasayansi wa nyuklia wa Iran na kusisitiza kuchukuliwa hatua waliohusika na jinai hiyo.
Habari ID: 3473405    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/29

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametilia mkazo wajibu wa kutiwa adabu na kupewa adhabu isiyoepukika wote waliofanya na kuamrisha mauaji ya kigaidi ya mwanasayansi wa Ki iran i, Dk. Mohsen Fakhrizadeh.
Habari ID: 3473403    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/28

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
TEHRAN (IQNA) - Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amelaani vikali hujuma hiyo ya kigaidi na kuongeza kuwa, kuna dalili nzito zinazoonyesha kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel ulihusika katika mauaji ya Mohsen Fakhrizadeh ambaye alikuwa Mkuu wa Shirika la Utafiti na Ubunifu katika Wizara ya Ulinzi ya Iran.
Habari ID: 3473401    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/28

Siku kama ya leo miaka 1241 iliyopita inayosadifiana na tarehe 10 Rabiuthani mwaka 201 Hijria, alifariki dunia Bibi Fatima Maasuma A.S, binti wa Imam Musa bin Jaafar A.S mmoja wa wajukuu watukufu wa Bwana Mtume Muhammad SAW.
Habari ID: 3473397    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/26

Mkuu wa zamani wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Ghana
TEHRAN (IQNA) – Jerry Rawlings, Rais wa zamani wa Ghana ambaye amefariki hivi karibuni akiwa na umri wa miaka 73, alikuwa mwanasiasa Mkristo ambaye aliathiriwa na kuiga baadhi ya fikra za Mapinduzi ya Kiislamu.
Habari ID: 3473388    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/24

Zarif katika Twitter baada ya
TEHRAN (IQNA) - Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran kwa mara nyingine tena inatangaza kwamba iko tayari kushirikiana na nchi za eneo hili kwa ajili kulinda na kufanikisha manufaa ya pamoja.
Habari ID: 3473344    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/09

TEHRAN (IQNA) – Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amenukulu aya za Qur’ani Tukufu katika Surah An-Naziat katika kufafanua kushindwa Donald Trump katika uchaguzi wa rais Marekani mwaka huu.
Habari ID: 3473342    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/08

Rais Rouhani wa Iran
TEHRAN (IQNA) - Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema taifa hili halijalishwi wala kushughulishwa na ni nani atakayeibuka mshindi katika uchaguzi wa rais wa Marekani uliofanyika jana Jumanne.
Habari ID: 3473328    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/04

TEHRAN (IQNA)- Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia ujumbe marais wa nchi za Kiislamu akiwapongeza kwa mnasaba wa kuadhimisha Maulidi na siku ya kuzaliwa Mtume wa mwisho wa Mwenyezi Mungu na Nabii wa rehma, upendo na amani, Muhammad SAW.
Habari ID: 3473324    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/03

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei atahutubu kwa njia ya televisheni kwa mnasaba wa maadhimisho ya kukumbuka siku ya kuzaliwa (Maulid) Mtume Muhammad SAW na pia uzawa wa mjukuu wake, Imam Jaafar Swadiq AS.
Habari ID: 3473318    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/01

TEHRAN (IQNA) - Mshauri wa sera za kigeni wa Spika wa Bunge la Iran ameashiria mauaji ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ambaye aliuawa kigaidi kufuatia amri ya rais Donald Trump wa Marekani na kusema, Trump ni gaidi nambari moja duniani.
Habari ID: 3473315    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/31

TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu ametilia mkazo udharura wa kuundwa kituo maalumu cha za Kiislamu kwa ajili ya kukabiliana na maafa katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 3473312    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/31

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu akiwahutubu vijana Wafaransa
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameeleza kushangazwa kwake na undumakuwili wa Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kwa kulikingia kifua jarida la Charlie Hebdo la nchini hiyo ya Ulaya kwa kuchapisha tena vibonzo vya kumvunjia heshima Mtume Muhammad SAW, kwa kisingizio cha uhuru wa kujieleza.
Habari ID: 3473306    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/29

TEHRAN (IQNA) - Mkutano wa 34 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu unatazamiwa kuanza Alhamisi kwa njia ya intaneti ambapo mada kuu itakuwa 'Ushirikiano wa Kiislamu Wakati wa Maafa na Majanga'.
Habari ID: 3473300    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/27