TEHRAN (IQNA- Balozi Mdogo wa Ufaransa mjini Tehran, Florent Aydalot, ameitwa katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kukabidhiwa malalamiko ya Iran kuhusu sisitizo la serikali ya Ufanrasa la kuwaunga mkono waliochapisha katuni zilizomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW.
Habari ID: 3473299 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/27
Spika wa Bunge la Iran
TEHRAN (IQNA) - Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, amesema nuru ya Mtume Mtukufu wa Uislamu, SAW, haiwezi kuzimwa kwa njama za maadui wa Kiislamu na kwamba njama hizo zitarejea kuwadhuru wao wenyewe.
Habari ID: 3473296 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/26
TEHRAN (IQNA) – Kituo cha Utamaduni cha Iran huko Pretoria, Afrika Kusini kimepanga mkutano wa umoja wa Kiislamu kwa njia ya intaneti maarufu kama webinar.
Habari ID: 3473285 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/22
Mkuu wa ICRO
TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Shirika la Utamaduni na Uhusiano wa Kiislamu Iran (ICRO) amesema, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) inapaswa kutekeleza majukumu yake kuhusiana na Fatuwa ambayo imetolewa na wanazuoni wa Kiislamu ya kuharamisha kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3473281 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/21
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Ukuras wa Twitter wa Kiongozi Maudhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu umezungumzia hatua ya baadhi ya nchi za Kiarabu ya kutangaza uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3473280 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/21
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema nchi hii katu haitafanya mazungumzo kuhusu uwezo wa makombora yake ya kujihami.
Habari ID: 3473275 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/19
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, sababu ya makelele na bwabwaja za wahuni wapayukaji nchini Marekani kuhusiana na uwezo wa kiulinzi, makombora na kieneo wa Iran ni kwamba, wahusika wametambua mahesabu makini na ya kiakili ya taifa hili kwa ajili ya kufikia uwezo huu.
Habari ID: 3473254 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/12
TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Wahadhiri katika Chuo cha Kiislamu cha Qum, nchini Iran imelaani vikali pendekezo la serikali ya Ufaransa la kuweka vizingiti katika harakati za Kiislamu nchini humo.
Habari ID: 3473250 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/11
Rais Hassan Rouhani
TEHRAN (IQNA)- Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani haitaweza kuvunja mapambano na muqawama wa taifa la Iran kwa kuweka vizingiti vya kununua na kudhamini dawa na chakula.
Habari ID: 3473244 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/09
TEHRAN (IQNA) – Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa na kusema jina za utawala wa Kizayuni wa Israel zimechupa mipaka.
Habari ID: 3473219 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/01
TEHRAN (IQNA) - Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nchi za Nje ya Iran amejibu madai ya uongo yaliyotolewa na Saudi Arabia ikisema kuwa imenasa kundi la magaidi lenye mfungamano na Iran na kusema: Watawala wa Saudia wanapaswa kuchagua njia ya ukweli hekima na busara badala ya kueneza uzusha na imlaa wanazopewa na madola mengine.
Habari ID: 3473217 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/30
Kamanda Mkuu wa IRGC
TEHRAN (IQNA) - Meja Jenerali Hussein Salami, Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) amesema kuwa, tadbiri na busara za Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu zimefelisha njama na malengo ya kisiasa ya adui katika Ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 3473214 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/29
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezitaka nchi za Armenia na Azerbaijan zijizuie na zisitishe mapigano yanayoshuhudiwa katika mpaka wa nchi mbili hizo tokea jana Jumapili.
Habari ID: 3473210 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/28
TEHRAN (IQNA) – Mkuu wa Idara ya Masuala ya Qur’ani katika Shirika la Wakfu la Iran amesema mashindano ya kitaifa ya Qur’ani nchini Iran mwaka huu yatafanyika kwa njia ya intaneti.
Habari ID: 3473207 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/27
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran akihutubu katika mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
TEHRAN (IQNA) - Rais Hassan Rouhani amesema: "Marekani haiwezi kutulazimisha kufanya mazungumzo wala kuanzisha vita dhidi yetu" na akasisitiza kwamba, sasa ni wakati wa walimwengu kusema "la" kwa ubabe na utumiaji mabavu.
Habari ID: 3473196 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/23
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezungumzia ushindi mkubwa na wa wazi wa taifa la Iran katika Vita vya Kujitetea Kutakatifu na kusema kuwa: Kujitetea kutakatifu ni sehemu ya utambulisho wa kitaifa wa Iran.
Habari ID: 3473189 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/21
TEHRAN (IQNA)- Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo Jumapili imetoa tamko rasmi na kusema kuwa, Marekani ndiye mhatarishaji mkubwa wa usalama na amani katika kona zote za dunia.
Habari ID: 3473186 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/20
Kwa mnasaba wa Maulidi ya Bwana Mtume Muhammad SAW
TEHRAN (IQNA) – Mkutano wa 34 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu utafanyika Novemba 11-13 katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Tehran.
Habari ID: 3473178 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/17
TEHRAN (IQNA) - Mkutano wa 13 wa Baraza la Kimataifa la Mwamko wa Kiislamu umefanyika katika mji mkuu wa Iran, Tehran kwa lengo la kujadil namna nchi kadhaa za Kiarabu zilivyowasaliti Wapalestina kwa kuanzisha uhusiano na utawala dhalimu wa Israel unaokalia ardhi za Palestina kwa mabavu.
Habari ID: 3473177 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/17
Rais Rouhani wa Iran
TEHRAN (IQNA) - Rais Hassan Rouhani wa Iran ameashiria pia kuanzishwa uhusiano wa kawaida baina ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Bahrain na utawala haramu wa Israel na kusema kuwa, watawala wa baadhi ya mataifa ya Kiarabu katika Asia Magharibi hawafungamani na malengo ya taifa madhulumu la Palestina.
Habari ID: 3473176 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/16